UKWELI KUHUSU MTI ULIOGOMA KUNG'OLEWA JIJINI MWANZA

George Binagi-GB Pazzo @BMG Wakazi wa Jiji la Mwanza wameingia katika taharuki baada ya kutokea uvumi wa taarifa za mti kugoma kung’ole...


George Binagi-GB Pazzo @BMG

Wakazi wa Jiji la Mwanza wameingia katika taharuki baada ya kutokea uvumi wa taarifa za mti kugoma kung’olewa katika eneo la Pasiansi ambapo kuna shughuli ya upanuzi wa barabara inayoelekea uwanja wa ndege wa Mwanza.


Taharuki hiyo ilianza tangu jana majira ya jioni ambapo mamia ya wananchi walijazana katika eneo hilo ili kushuhudia mgomo wa mti huo ambao inasadikika ulikuwa ukitoa sauti za kulalama mithiri ya binadamu.


Zoezi la kuung’oa mti huo aina ya mwembe limefanikiwa hii leo majira ya saa tatu asubuhi baada ya shughuli pevu ya kuung’oa kwa kutumia mashine aina ya burudoza huku baadhi wakihusisha tukio hilo na imani za kishirikina na wengine wakisema ni upotoshaji tu ulifanyika juu ya tukio hilo.


Kasim Mlisu ambaye ni mfanyakazi wa kampuni ya ujenzi ya Nyanza Road Works inayojenga barabara ya Pasiansi, amesema taarifa za mti huo kuzungumza ni za upotoshaji na kwamba zoezi la kuung’oa lilichukua muda mrefu tangu juzi ili kupisha hatua za upimaji wa ukubwa wake na kusubiri mashine aina ya“skaveta” iliyofanikiwa kuung’oa.


Katibu wa Chama cha Tiba asilia mkoani Mwanza CHAWATIATA, Kawawa Athuman, amesema tukio la mti kuzungumza ama kugoma kung’olewa halina ukweli wowote kwa karne hii ya 21 japo matukio ya aina hiyo yalikuwepo enzi za kale kabla ya ujio wa dini barani Afrika ambapo amewatahadharisha watumiaji wa mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kujiepusha na usambazaji wa taarifa za upotoshaji.

Zoezi la kuung'oa mti likiendelea
Hapa msumeno ulikata ila mti ukagoma kuangua licha ya kuvutwa
Zoezi la kuung'oa mti huo likiwa limefanikiwa
Zoezi la kuung'oa mti huo likiwa limefanikiwa
Zoezi la kuung'oa mti huo likiwa limezaa matunda
Katibu wa Chama cha Tiba asilia mkoani Mwanza CHAWATIATA, Kawawa Athuman, akizungumzia tukio hilo
Kasim Mlisu ambaye ni mfanyakazi wa kampuni ya ujenzi ya Nyanza Road Works akizungumzia tukio hilo
Mkazi wa jiji la Mwanza akizungumzia tukio hilo
Wakazi wa jiji la Mwanza wakifuatilia tukio hilo
Wakazi wa jiji la Mwanza wakichukua tukio hilo
Wanahabari na wakazi wa jiji la Mwanza wakichukua tukio hilo
Wanahabari na wakazi wa jiji la Mwanza wakichukua tukio hilo
Kushoto ni dereva aliyekuwa akiendesha mtambo uliong'oa mti huo

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: UKWELI KUHUSU MTI ULIOGOMA KUNG'OLEWA JIJINI MWANZA
UKWELI KUHUSU MTI ULIOGOMA KUNG'OLEWA JIJINI MWANZA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjmFPv3EC4M_d8aadsc7vQrNfYa5yc0FoZ2L-Z1qlZkcirddJvPVUpKyYuk5iyWRoaBoIyUy_F-WsAcjhaEVnWl3xjDGKeOOGhTwnag8QcKwwXna70KxOkkAJ0sblc0C_B9jL5pM-7Vf3s/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjmFPv3EC4M_d8aadsc7vQrNfYa5yc0FoZ2L-Z1qlZkcirddJvPVUpKyYuk5iyWRoaBoIyUy_F-WsAcjhaEVnWl3xjDGKeOOGhTwnag8QcKwwXna70KxOkkAJ0sblc0C_B9jL5pM-7Vf3s/s72-c/1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/ukweli-kuhusu-mti-uliogoma-kungolewa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/ukweli-kuhusu-mti-uliogoma-kungolewa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy