Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Injinia Enocent Msasi akizungumza katika mkutano na wanahabari leo kuzung...
SHIRIKA la
Trust Care Tanzania Foundation kwa kushirikiana na Kampuni ya Simu
Tanzania (TTCL) wameandaa semina ya kuwajengea uwezo wa kifikra
wanafunzi wa vyuo vikuu mbalimbali vya jijini Dar es Salaam ikiwa na
lengo la kuwabadili wanafunzi kwa ujumla kuwa na mawazo chanya
yatakayowawezesha kutumia fursa anuai zinazowazunguka katika jamii mara
baada ya masomo yao.
Akizungumzia
semina hiyo inayotarajiwa kufanyika Jumamosi ya tarehe 20/05/2017
katika ukumbi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam (DUCE) kuanzia
majira ya saa tatu asubuhi, Mkurugenzi Mtendaji wa Trust Care Tanzania
Foundation, Zambert Mbwafu alisema semina hiyo ni maalum kwa wanafunzi
waliopo vyuoni kwa ajili ya kuwajengea uwezo.
Alizitaja
mada ambazo wanafunzi wanatarajia kufundishwa ni pamoja na Umuhimu wa
Kujiamini na Kujijengea Uwezo, Uwezo wa Uthubutu, Vipaji na Jinsi ya
Kuviendeleza, Maadili na Nidhamu katika Kazi na Ubunifu katika Kufikia
Malengo. "Semina inawaandaa vijana waliopo na ambao wanatarajia kumaliza
elimu yao ya juu hivi karibuni kupata elimu na ujuzi utakaowasaidia
wakiwa shule na baada ya kumaliza masomo yao ili waweze kwenda sambamba
na mahitaji ya ulimwengu wa sasa..." alisema Bw. Mbwafu.
Akifafanua
zaidi Mkurugenzi, Zambert Mbwafu, alivitaja vyuo vitakavyoshiriki
katika semina hiyo; ni pamoja IFM, CBE, DIT, DUCE, TIA, UDSM, MUHAS,
CHUO CHA DIPLOMASIA, KIU, CHUO CHA USTAWI WA JAMII NA CHUO KIKUU CHA
TUMAINI.
Kwa
upande wa wadhamini wakuu wa semina hiyo Kampuni ya TTCL, Injinia
Enocent Msasi Mkurugenzi wa Biashara TTCL alisema kampuni hiyo inaunga
mkono kampuni ya Trust Care Tanzania kwa dhumuni lake la kuisaidia jamii
katika maeneo mbalimbali, ikiwemo sekta za kiafya, kielimu na kijamii.
Aliongeza kuwa lengo hilo linashabihiana na lengo la TTCL kuhakikisha
inakuwa na jamii bora zaidi kiteknolojia, kielimu, kiafya na kimaendeleo
kwa ujumla.
"TTCL
imedhamini semina hii kwasababu inatoa mchango mkubwa katika kujenga
taifa lenye vijana wachapakazi, vijana wenye mtizamo chanya, vijana
wenye uwezo wa uthubutu, na kupambana na changamoto mbalimbali za
kimaisha, " alisema Msasi na kuongeza kuwa TTCL kupitia huduma zake bora
za intaneti, sauti na SMS inawaunga mkono vijana mara zote na itakuwa
mstari wa mbele kufanikisha juhudi zao za kuleta mabadiliko chanya
katika jamii.
"TTCL
kwa miaka mingi tumekuwa tukipokea vijana wanaokuja kufanya mafunzo kwa
vitendo kutoka vyuo na taasisi mbalimbali za elimu zinazotoa elimu
katika fani tofauti tofauti. Lakini safari hii tumekuja kivingine zaidi,
kwa kuja na programu ambayo itasaidia vijana kupata uzoefu baada ya
kumaliza masomo yao. Hii itasaidia kuondoa changamoto ya vijana wetu
waliomaliza elimu ya juu ambao mara nyingi hupoteza fursa mbalimbali za
ajira kwa kukosa sifa ya uzoefu."
Vijana
watakao pata fursa ya kufanya kazi na TTCL watajifunza mengi kawa
vitendo huku wakiongozwa kwa wataalamu wabobezi katika fani mbalimbali.
Tunaamini watakapomaliza programu hiyo vijana hao watapata fursa kupata
ajira kwenye taasisi na makampuni mbalimbali, au kujiajiri wenyewe,"
alisisitiza Enocent Msasi akizungumza na wanahabari leo.
COMMENTS