TIMU YA AZANIA YAKWEA PIPA KUELEKEA UINGEREZA

Timu ya Azania imeondoka nchini kuelekea Uingereza kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Standard Chartered Safari kwenda Anfield yatakay...

Timu ya Azania imeondoka nchini kuelekea Uingereza kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Standard Chartered Safari kwenda Anfield yatakayofanyika kwenye uwanja wa klabu ya Liverpool wa Anfield.
Timu hiyo imeondoka na msafara wa watu 10 ambapo kati yao wachezaji ni saba ambao ni Shabaka Hamisi, Rajabu Ally, Akhamedy Afifu, Abdalah Khalid, Thomas Bishanga, Alidi Said na Brayan Dobadi.
Wachezaji wa Timu ya Azania wakibadilishana mawazo mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere tayari kukwea pipa kuelekea nchini Uingereza.
Azania itashiriki mashindano hayo ikiwa ni mabingwa wa kombe la Standard Chartered Safari kwenda Anfield kwa Afrika Mashariki na Kati na ikiwa kwenye mashindano hayo itakutana na timu zingine kutoka Botswana, Nigeria, Hong Kong, Korea, Singapore, India pamoja na Uingereza.
Timu hiyo itafika Uingereza Mei, 19 wakiwa huko watakutana na timu zingine, Mei, 20 watatembelea uwanja wa Anfield, Mei, 21 watashuhudia mchezo wa Liverpool na Middlesbrough na baada ya hapo wataingia uwanjani kwa ajili ya mashindano na watarejea nchini Mei, 22.
Mariam Sezinga (kushoto) wa Benki ya Standard Chartered Tanzania akiongoza msarafa huo wa timu ya Azania kuelekea nchini Uingereza.
Kikosi cha Timu ya Azania katika picha ya pamoja na kiongozi wa msafara huo Mariam Sezinga (wa kwanza kushoto) wa Benki ya Standard Chartered nchini kabla ya kuingia lango kuu la kusafiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Timu ya Azania wakiingia ku-'check in' tayari kukwea pipa kuelekea nchini Uingereza.
Mariam Sezinga (kulia) wa Benki ya Standard Chartered Tanzania akihakikisha hati zote zimekamilika tayari kwa ku-'check in' katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Timu ya Azania wakiwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa Dubai usiku wa kuamkia leo safarini kuelekea nchini Uingereza.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TIMU YA AZANIA YAKWEA PIPA KUELEKEA UINGEREZA
TIMU YA AZANIA YAKWEA PIPA KUELEKEA UINGEREZA
https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEhFgm0iSXXO1IubZfHLluzKLB1KJ3P1nb63Oi-0FBjP0bi6QFf0sIEGr4Xyipa6i8S9GD_Tm-ysG5k6ail0egSTLPOJWXI8g5wdCnj9YpnI4OIncQKZDnoLLSom6MMZmfjEXF912dmyZ-VyaeLTVyoDSoLTupcIOrb6gDWURCslTk6a=s0-d-e1-ft
https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEhFgm0iSXXO1IubZfHLluzKLB1KJ3P1nb63Oi-0FBjP0bi6QFf0sIEGr4Xyipa6i8S9GD_Tm-ysG5k6ail0egSTLPOJWXI8g5wdCnj9YpnI4OIncQKZDnoLLSom6MMZmfjEXF912dmyZ-VyaeLTVyoDSoLTupcIOrb6gDWURCslTk6a=s72-c-d-e1-ft
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/timu-ya-azania-yakwea-pipa-kuelekea.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/timu-ya-azania-yakwea-pipa-kuelekea.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy