Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe ameikabidhi bendera timu ya Azania ambayo inaelekea nchini Uinger...
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe ameikabidhi bendera timu ya Azania
ambayo inaelekea nchini Uingereza kushiriki mashindano ya Standard
Chartered Safari kwenda Anfield.
Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi bendera pamoja na hati za
kusafiria, Waziri Mwakyembe alisema ni fursa ya kipekee ambayo Tanzania
imeipata kushiriki mashindano kama hayo na ni muda sasa dunia kujua kuwa
Tanzania kuna vipaji vya soka hivyo wahakikishe wanarudi nchini na
kikombe.
“Mtuwakilishe vyema huko muendako ni muda sasa wa dunia kuwa
Tanzania tuna uwezo wa kisoka, kila mmoja acheze vizuri na kuonyesha
uwezo wake, tunaamini mtarudi na kikombe na nawatakia kila la kheri,” alisema Waziri Mwakyembe. Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe
akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi bendera pamoja na hati za
kusafiria kwa timu ya Azania ambayo inaelekea nchini Uingereza kushiriki
mashindano ya Standard Chartered Safari kwenda Anfield iliyofanyika
katika hoteli ya Southern Sun jijini Dar Es Salaam.[/caption]
Nae Mjumbe wa Bodi ya Standard Chartered Tanzania, Ami Mpungwe amesema
benki yao inajivunia kupata wawaklishi kutoka Tanzania na wamesimamia
gharama zote za safari kwa muda wote ambao timu itakuwa Uingereza na ni
matumaini yao kuwa timu hiyo ya Azania itarejea nchini na kikombe.
“Tupo hapa kuiaga timu ya Azania ambao ni mabingwa wa Tanzania na Afrika
Mashariki wa kombe la Standard Chartered Safari kwenda Anfield,
tunajivunia timu hii sababu imetuletea heshima kubwa, tunawaombe ushindi
mkubwa na tunategemea watakuja na ubingwa,” alisema Mpungwe. Balozi
wa Uingereza nchini, Sarah Cooke akitoa pongezi kwa timu ya Azania
kupata nafasi ya kwenda Uingereza wakati wa hafla ya kukabidhi bendera
kwa timu hiyo inayokwea pipa kesho 18 Mei. Kushoto ni Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe.[/caption]
Kwa upande wa Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke aliipongeza timu
ya Azania kwa kupata nafasi ya kwenda Uingereza kucheza kwenye moja ya
kiwanja maarufu cha Anfield lakini pia kuipongeza benki ya Standard
Chartered kwa kufikisha miaka 100 tangu kuanza kutoa huduma nchini.
“Hii ndiyo nguvu ya michezo inauwezo wa kuwaunganisha watu pamoja,
mnakwenda Uingereza tunaijua ni timu kubwa nawapongeza Azania kwa kupata
nafasi, hongereni sana nawatakia kila la kheri najua mtafurahi kwa
kipindi ambacho mtakuwa kule,
“Mnakwenda kwenye moja ya uwanja maarufu nchini Uingereza, Liverpool ni
timu yenye historia na wachezaji wakubwa kama Steven Gerarld, Kenny
Dalglish na wengine wengi, pia niwapongeze Standard Chartered kwa
kufikisha miaka 100 tangu kuanza kufanya kazi Tanzania,” alisema Cooke. Mkuu
wa idara ya Fedha wa Benki ya Standard Chartered, Abdulrahman Said
akizungumzia safari ya timu ya Azania katika hafla ya kukabidhi bendera
kwa timu hiyo inayokwea pipa kesho 18 Mei kuelekea nchini
Uingereza.[/caption]
Nae nahodha wa timu hiyo, Khalid Sultan Said aliahidi kuwa timu hiyo
inajiamini kuwa inauwepo wa kupambana na timu zingine na kuahidi kuwa
itahakikisha kikombe kinakuja nchini.
Timu hiyo itaondoka nchini Mei, 18 watafika Mei, 19 wakiwa huko
watakutana na timu zingine, Mei, 20 watatembelea uwanja wa Anfield, Mei,
21 watashuhudia mchezo wa Liverpool na Middlesbrough na baada ya hapo
wataingia uwanjani kwa ajili ya mashindano na watarejea nchini Mei, 22. Mjumbe
wa Bodi ya Standard Chartered Tanzania, Ami Mpungwe (kushoto)
akizungumzia wakati wa halfa ya kukabidhi bendera timu ya Azania
inayotarajia kukwea pipa kesho Mei 18 kuelekea nchini Uingereza. Kulia
ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison
Mwakyembe. Nahodha
wa timu ya Azania, Khalid Sultan Said akizungumza na waandishi wa
habari wakati wa hafla ya kukabidhiwa bendera kuelekea nchini Uingereza
kesho Mei 18. Kikosi cha Timu ya Azania katika hafla ya kukabidhiwa bendera kuelekea nchini Uingereza kesho Mei 18. Picha
juu na chini ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk.
Harrison Mwakyembe akiabidhi hati za kusafiria kwa wachezaji wa timu ya
Azania wanaotarajia kukwea pipa kesho Mei 18 kuelekea nchini
Uingereza.Katikati ni Mkuu wa Mahusiano wa Benki ya Standard Chartered, Juanita Mramba.
Balozi
wa Uingereza nchini, Sarah Cooke akikabidhi hati ya kusafiria kwa
mwandishi wa TV1 atakayeambatana na msafara wa timu hiyo kuelekea nchini
Uingereza.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (wa pili
kulia) akikabidhi rasmi bendera kwa Nahodha wa timu ya Azania, Khalid
Sultan Said. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mjumbe wa Bodi ya Standard
Chartered Tanzania, Ami Mpungwe (suti nyeusi) na Balozi wa Uingereza
nchini, Sarah Cooke (kulia). Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe
akimkabidhi jezi Nahodha wa timu ya Azania, Khalid Sultan Said wakati wa
hafla ya kukabidhi bendera timu hiyo. Katikati ni Mjumbe wa Bodi ya
Standard Chartered Tanzania, Ami Mpungwe.
COMMENTS