Na Benny Mwaipaja, WFM. Serikali za Tanzania na Uganda zimetiliana saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la k...
Na Benny Mwaipaja, WFM.
Serikali
za Tanzania na Uganda zimetiliana saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa
Bomba la Mafuta Ghafi la kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga nchini
Tanzania lenye urefu wa Kilometa 1,443, uliokadiriwa kugharimu zaidi ya
Dola bilioni 3 nukta 55, mjini Kampala Uganda, leo.
Mkataba
huo umesainiwa na Waziri wa Katiba na Sheria wa Tanzania, Profesa
Paramagamba Kabudi na Waziri wa Nishati wa Uganda, Mhandisi Irene
Muloni.
Tukio
hilo limekuja siku chache baada ya Marais wa Nchi hizo mbili, Dkt. John
Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Uganda Yoweri Kaguta Museveni,
kutia saini tamko la pamoja la kukamilika kwa majadiliano ya vipengele
vya mkataba, Ikulu Jijini Dar es salaam.
Hafla
ya kutia saini Mkataba huo iliyofanyika katika Hoteli ya Serena, Jijini
Kampala, Uganda imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa nchi zote mbili
wakiwemo Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wanasheria Wakuu wa Serikali,
Wakurugenzi na Viongozi wa taasisi mbalimbali zinazohusika katika mradi
huo.
Mradi
wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima-Uganda hadi Tanga Tanzania,
unatarajia kusisimua uchumi wa nchi hizo mbili na katika mchakato wa
ujenzi wake zaidi ya watu 10,000 wanatarajiwa kunufaika na ajira.
Hivi
Karibuni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe
Magufuli aliuelezea mradi huo kuwa ni mkubwa kwakuwa Uganda imegundua
shehena kubwa ya mafuta katika eneo la Hoima kiasi cha mapipa bilioni 6
na laki 5 na kwamba Tanzania inatarajia pia kupata mafuta kule ziwa
Tanganyika na ziwa Eyasi, ambayo yatapitishwa katika bomba hilo hilo.
Waziri
wa Katiba na Sheria wa Tanzania, Profesa Paramagamba Kabudi (kulia) na
Waziri wa Nishati wa Uganda, Bi. Irene Muloni (kushoto) wakitia saini
Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini
Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania, tukio lililofanyika leo
katika Hoteli ya Serena, Kampala, Uganda
Waziri
wa Katiba na Sheria wa Tanzania, Profesa Paramagamba Kabudi (kulia) na
Waziri wa Nishati wa Uganda, Bi. Irene Muloni (kushoto) wakitia saini
Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini
Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania, tukio lililofanyika leo
katika Hoteli ya Serena, Kampala, Uganda
Ujumbe
wa Tanzania na Uganda ukishuhudia tukio la utiwaji saini wa Mkataba wa
Ujenzi wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi
Bandari ya Tanga nchini Tanzania, tukio lililofanyika leo katika Hoteli
ya Serena, Kampala, Uganda.
Waziri
wa Katiba na Sheria wa Tanzania, Profesa Paramagamba Kabudi, akihutubia
baada ya kutia saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa Bomba la Mafuta
Ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania,
tukio lililofanyika leo katika Hoteli ya Serena, Kampala, Uganda.
Mwanasheria
Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Bw. George Masaju (kulia) na Mwanasheria
wa Uganda Bw. Milliam Byaruhanga (kushoto), wakionesha nakala za Mkataba
wa Ujenzi wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini Uganda
hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania, tukio lililofanyika leo katika
Hoteli ya Serena, Kampala, Uganda.
Waziri
wa Katiba na Sheria wa Tanzania, Profesa Paramagamba Kabudi (kulia) na
Waziri wa Nishati wa Uganda, Bi. Irene Muloni (kushoto) wakionesha
Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini
Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania, baada ya kuusaini, tukio
lililofanyika leo katika Hoteli ya Serena, Kampala, Uganda.
COMMENTS