SERIKALI IMEKUSANYA BILIONI 63 KUPITIA MTAMBO WA KUHAKIKI NA KUSIMAMIA HUDUMA ZA MAWASILIANO YA SIMU NCHINI

Na Daudi Manongi-MAELEZO, DODOMA. Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) imekusanya shilingi bilioni 63,015...


Na Daudi Manongi-MAELEZO, DODOMA.

Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) imekusanya shilingi bilioni 63,015,450,230 kwa kipindi cha Octoba 2013 mpaka Februari 2017 tangu kuanzishwa kwa mtambo wa kuhakiki na kusimamia Huduma za Mawasiliano(TTMS) nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Edwin Ngonyani wakati akijibu swali la Mbunge wa Kigamboni Mhe. Dkt Faustine Engelbert leo Bungeni.

“Mtambo huu umesaidia Mamlaka ya Mawasiliano nchini kuongeza ufanisi katika kusimamia Sekta ya Mawasiliano pamoja na kwenda sambamba na kasi ya mabadiliko yanayotokea katika Sekta ya Mawasiliano Duniani kote”,Aliongeza Mhe.Ngonyani.

Aidha kati ya pesa izo bilioni 56,987,368,631 zimewasilishwa hazina na shilingi bilioni 6,028,081,599 zimewasilishwa Tume ya Sayansi na Teknolojia(COSTECH) kwa ajili ya kugharamia tafiti mbalimbali zenye manufaa kwa nchi yetu ambapo kabla ya hapo kahukuwa na mapato hayo.

Amesema mtambo huu umeiwezesha TCRA kuwa na uwezo wa kusimamia mawasiliano ya simu za Kimataifa na zile za mwingiliano,pia mtambo huo umesaidia kudhibiti mawasiliano ya Simu za ulaghai za kimataifa na kusimamia ubora wa mitandao katika kutoa huduma bora kwa wananchi,kudhibiti namba tambulishi za vifaa vya mawasiliano nchini pamoja na usimamiaji wa miamala ya fedha  inayopita katika mitandao ya simu hapa nchini.

“Aidha pamoja na mafanikio hayo jitihada za kuboresha zaidi mfumo huu ili kuweza kubaini na kujiridhisha juu ya mapato yote yatokanayo na huduma za  mawasiliano na yanayokidhi mahitaji ya Mamlaka ya Mapato Tanzania,Benki kuu ya Tanzania na TCRA zinaendelea”Aliongeza Mhe. Ngonyani.

Aidha Serikali itaendelea kuwajengea uwezo wataalamu wa TCRA ili waweze kuendana na kasi ya ukuaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano hususani katika eneo hili la kuchakata taarifa mbalimbali za huduma za mawasiliano zinazopatikana kutoka kwa watoa huduma ili kuweza na kujiridhisha juu ya mapato yote.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SERIKALI IMEKUSANYA BILIONI 63 KUPITIA MTAMBO WA KUHAKIKI NA KUSIMAMIA HUDUMA ZA MAWASILIANO YA SIMU NCHINI
SERIKALI IMEKUSANYA BILIONI 63 KUPITIA MTAMBO WA KUHAKIKI NA KUSIMAMIA HUDUMA ZA MAWASILIANO YA SIMU NCHINI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgZ1oUZecxCAXKZaBsB1gWURq3SXWBzsFqrL47b8tF1CqRtYjIKsD7NOY1bh2aV-hKerRWT_4OHH-fVxTyHOtuIgs7HvlWgJTepzfXwefk9y3-Y5wXr7CcMCOyLCs5BtjbdTc5smrsi_auA/s320/8406-Mhe.Ngonyani+1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgZ1oUZecxCAXKZaBsB1gWURq3SXWBzsFqrL47b8tF1CqRtYjIKsD7NOY1bh2aV-hKerRWT_4OHH-fVxTyHOtuIgs7HvlWgJTepzfXwefk9y3-Y5wXr7CcMCOyLCs5BtjbdTc5smrsi_auA/s72-c/8406-Mhe.Ngonyani+1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/serikali-imekusanya-bilioni-63-kupitia.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/serikali-imekusanya-bilioni-63-kupitia.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy