NEWZ ALERT:MALIMA NA DEREVA WAKE WAFIKISHWA MAHAKAMA YA KISUTU KWA TUHUMA ZA KUMSHAMBULIA ASKARI POLISI

Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii. Aliyekuwa Naibu Waziri wa fedha na mbunge wa Mkuranga, Adam Kigoma Malima amefikishwa mahakam...


Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Aliyekuwa Naibu Waziri wa fedha na mbunge wa Mkuranga, Adam Kigoma Malima amefikishwa mahakamani kujibu tuhuma za kumshambulia askari polisi.

Malima anashtakiwa pamoja na dereva wake Ramadhani Mohamed Kigwande anayekabiliwa na tuhuma za kujeruhi.

Washtakiwa wamesomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicious Mwijage wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Wakili wa serikali, Mwanaamina Kombakono amedai, Mei 15 mwaka huu huko Masaki katika wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam mshtakiwa Malima alitenda kosa.

Imedaiwa, siku hiyo mshtakiwa Malima alimzuia afisa wa polisi mwenye namba H.7818 PC Abdul kufanya kazi yake ya kumkamata dereva wake Kigwande aliyekuwa amefanya kosa la kumjeruhi Joseph Mwita ambaye ni afisa operation wa Priscane Business Enterprises.

Kombakono ameongeza kuwa, siku na mahali hapo, mshtakiwa Kigwande kwa nia ya kukataa kukamatwa, alimjeruhi afisa operation hiyo(Joseph Mwita) ambaye alikuwa anakamatwa kwa kosa la kupaki gari vibaya na kumsababishia Mwita Majeraha Mwilini.

Watuhumiwa wote wamekana kutenda makosa hayo na wako nje kwa dhamana.mahakama imemtaka kila mshtakiwa kuwa na mdhamini mmoja atakaye saini dhamana ya milioni 5. Aidha Mahakama imemtaka kila mdhamini awe na barua ya utambulisho kutoka ofisi yoyote inayotambulika.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 15, mwaka huu ambapo kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi bado haujakamilika.Wakili Kibatala ameieleza mahakama kuwa, tarehe ya kutajwa kwa kesi hiyo atawasilisha pingamizi la awali juu ya mapungufu ya kisheria yaliyopo kwenye shtaka la shambulio linalomkabili Malima Peke yake.

Amedai kuwa, katika shtaka hilo maelezo ya kosa na tuhuma hazifanani.


Aidha Hakimu Mwijage ameutaka upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi haraka." Hii siyo kesi ya kuchukua muda mrefu kukamilisha upelelezi, wahusika wote wapo, aliyejeruhiwa na waliojeruhi, mi nilitegemea mtakuja hapa na kusema upelelezi umekamilika", amesema Hakimu Mwijage

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: NEWZ ALERT:MALIMA NA DEREVA WAKE WAFIKISHWA MAHAKAMA YA KISUTU KWA TUHUMA ZA KUMSHAMBULIA ASKARI POLISI
NEWZ ALERT:MALIMA NA DEREVA WAKE WAFIKISHWA MAHAKAMA YA KISUTU KWA TUHUMA ZA KUMSHAMBULIA ASKARI POLISI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiEWshFvQ4oH2iY1sCX8WuJIugnyTB9YNdH8J4EtJ7SLwCoBUB9RRbSJpfZrYc0F6eBjbdwXm4zY3kimxoF3tTzos7xWC_mJHZhpUNa4WDVwZJvU4rRgE_vVkJxbFLfCY_jZq2uZAw2QZU/s400/2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiEWshFvQ4oH2iY1sCX8WuJIugnyTB9YNdH8J4EtJ7SLwCoBUB9RRbSJpfZrYc0F6eBjbdwXm4zY3kimxoF3tTzos7xWC_mJHZhpUNa4WDVwZJvU4rRgE_vVkJxbFLfCY_jZq2uZAw2QZU/s72-c/2.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/newz-alertmalima-na-dereva-wake.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/newz-alertmalima-na-dereva-wake.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy