Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe. Hamad Masauni akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest ...
Naibu
Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe. Hamad Masauni
akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu wakati
anawasili katika ukumbi wa mikutano wa AICC kwa ajili ya ufunguzi wa
Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za
kusini mwa Afrika (SARPCCO). Kulia ni Mkuu wa INTERPOL kanda ya Kusini
Mubita Nawa.
Katibu
Mtendaji wa SADC, Dk. Stegomena Tax akizungumza na Mkuu wa Jeshi la
Polisi nchini IGP Ernest Mangu kabla ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa
mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika
(SARPCCO) unaofanyika mkoani Arusha. IGP Mangu ndiye Mwenyekiti wa
shirikisho hilo kwa kipindi hiki.
Baadhi
ya Wakuu wa majeshi ya Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika SADC
wakitoa heshima wakati wimbo wa taifa unapigwa wakati wa hafla ya
ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi
kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) uliofanyika Mkoani Arusha.
IGP wa Tanzania, Ernest Mangu ndiye Mwenyekiti wa shirikisho hilo kwa
kipindi hiki.
Katibu
Mtendaji wa SADC, Dk.Stegomena Taxi, akitoa hotuba wakati wa hafla ya
ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi
kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) Mkutano huo ulifunguliwa na
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe.Hamad Masauni
Mkoani Arusha. IGP wa Tanzania Mangu ndiye Mwenyekiti wa shirikisho hilo
kwa kipindi hiki.
Naibu
Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe.Hamad Masauni akiwa
katika picha ya pamoja na Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa
afrika (SARPCCO) baada ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa
Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika
unaofanyika Mkoani Arusha.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP
Ernest Mangu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) akiwa
ameambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi la Angola, Paulo de Almeida
(kushoto) na Mkuu wa jeshi la Polisi la Msumbiji, Paulo Chachine (kulia)
wakati wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka
nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) uliofanyika Mkoani Arusha. (Picha na
Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi)
COMMENTS