Kampuni ya simu ya Mkononi ya Itel imemtambulisha Msanii Bongo Movis, Irene Uwoya kuwa Balozi wa kampuni hiyo hapa nchini. ...
Kampuni ya simu ya Mkononi ya Itel imemtambulisha Msanii Bongo Movis, Irene Uwoya kuwa Balozi wa kampuni hiyo hapa nchini.
Akizungumza
na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam, Irene amesema amejisikia
faraja kuwa balozi na kuahidi kuitendea kazi katika kutangaza kampuni
hiyo kupitia bidhaa zao za simu.
Amesema
kuwa amekuwa akifanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja na kuweza kufanya
makubaliano ya kuwa balozi katika kuunganisha itel na watanzania kwa
ujumla.
Kwa
upande Mkurugenzi wa Itel, Coopeer Chan amesema kuwa wanatarajia
jamii itafaidika kwa kupata elimu kuhusu bidhaa za kampuni hiyo kupitia
kwa balozi Irene Uwoya katika matukio ya kuonyesha ukarimu kwa baadhi
ya makundi kwa utoaji wa misaada.
Amesema kuwa wanamkaribisha balozi mpya itel Tanzania Irene Uwoya kuungana na familia ya kubwa ya itel.
"Sote
tunafahamu mchango wa Irene Uwoya kwenye jamii amekuwa akielimisha
kupitia filamu zake na kutambua umuhimu wake sisi itel Mobile
tutashirikiana naye kikamilifu kuhakikisha jamii inapata kile
inachotarajia kukipata kwetu na kwake pia" amesema Chan.
Mkuruegenzi
wa itel, Coopeer Chan akisaini makubaliano na Msanii Bongo Movis,
Irene Uwoya kuwa balozi wa kampuni hiyo leo katika ukumbi wa Hoteli ya
Hyaat Legency jijini Dar es Salaam.
Msanii
Bongo Movis ,Irene Uwoya akizungumza na waandishi wa habari juu kuwa
balozi wa Kampuni ya Simu ya Mkononi leo jijini Dar es Salaam.
Afisa
Masoko wa Itel, Asha Mzimbili akizungumza na waandshi habari juu
makubaliano katika balozi mpya itel, Irene Uwoya leo jijini Dar es
Salaam.
Mkuruegenzi
wa Itel , Coopeer Chan akibadilishana hati ya makubaliano na Msanii
Bongo Movis ,Irene Uwoya kuwa balozi wa kampuni hiyo leo katika ukumbi
wa Hoteli ya Hyaat Legency jijini Dar es Salaam.
Msanii Bongo Movis, Irene Uwoya akiwa katika picha ya pamoja wafanyakazi Itel leo jijini Dar es Salaam.
COMMENTS