DARAJA LA MAGARA KUANZA KUJENGWA MWEZI JULAI

Na Mwandishi Wetu Serikali imesema ipo katika hatua za mwisho za kumpata mkandarasi atakayejenga Daraja la Magara lenye urefu wa Mita 8...


Na Mwandishi Wetu
Serikali imesema ipo katika hatua za mwisho za kumpata mkandarasi atakayejenga Daraja la Magara lenye urefu wa Mita 84 katika barabara ya Mbuyu wa Mjerumani-Mbulu KM 21 lililopo mkoani Manyara ambapo mkataba huo unatarajiwa kusainiwa mwezi Juni mwaka huu.
Akizungumza hayo jana kwa wananchi wa Kijiji cha Mayoka, wilaya ya Babati, mkoani humo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, amewataka wananchi hao kutoa ushirikiano kwa mkandarasi atakayepatikana ili kurahisisha mradi huo kukamilika kwa wakati.
Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Manyara Eng. Bashiri Rwesingisa, akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, wakati alipokuwa akikagua mahali ambapo litajengwa Daraja la Magara lenye urefu wa Mita 84, Wilayani Babati, mkoani Manyara, jana.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, akitoa maelekezo kwa Mhandisi Christopher Saul (katikati), kutoka Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), mkoa wa Manyara wakati alipokuwa akikagua mahali ambapo litajengwa Daraja la Magara lenye urefu wa Mita 84, Wilayani Babati, mkoani humo, jana.

Muonekano wa Sehemu ambapo Daraja la Magara lenye urefu wa Mita 84 katika barabara ya Mbuyu wa Mjerumani-Mbulu KM 21 litakapojengwa. Mkataba wa ujenzi wake unatarajiwa kusainiwa mwezi Juni mwaka huu.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mayoka kuhusu mkakati wa Serikali katika ujenzi wa Daraja la Magara wilayani Babati, mkoani Manyara, jana.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini cha Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano)

"Serikali inaendelea kukamilisha taratibu zake ili kumpata mkandarasi, sasa ombi langu kwenu ni kuhakikisha kuwa mnatoa ushirikiano kwa Mkandarasi huyo pindi atakapofika eneo la kazi", amesema Naibu Waziri.
Amebainisha kuwa Serikali imekuwa ikitenga fedha mwaka hadi mwaka ili kuweza kukamilisha mradi huo ambapo kwa mwaka wa fedha 2017/18 zaidi ya Shilingi Bilioni 1 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa KM 1.2 za barabara sehemu ya mlima Magara ambayo itajengwa kwa kiwango cha zege.
Naye, Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Manyara Eng. Bashiri Rwesingisa amemhakikishia Naibu Waziri huyo kumsimamia mkandarasi atakayepatikana katika ujenzi wa Daraja hilo ili kuondoa kero na adha wanayopata wakazi wa Babati na maeneo jirani.
Ameongeza kuwa ujenzi wa Daraja la Magara pia litahusisha ujenzi wa barabara unganishi zenye urefu wa KM 2 kwa kiwango cha lami na KM 2 kwa kiwango cha Changarawe.
Daraja la Magara ni moja ya Daraja litakaloleta chachu ya maendeleo kwa wakazi wa Arusha, Mbulu na Babati kwani ujenzi wake utarahisisha huduma za usafirishaji na kukuza utalii kwa nchi kupitia Hifadhi ya Mbuga ya Manyara.
(Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano)

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: DARAJA LA MAGARA KUANZA KUJENGWA MWEZI JULAI
DARAJA LA MAGARA KUANZA KUJENGWA MWEZI JULAI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhVrTsLPtoqzR3H3RlVwJtIWnCbe8pCP2vMh_UeUVfdmb2m3Tdn6vHdO4MKVnNH9zAmcPn5TglLrzi89tieT0411XIUTXpv7XZo66jtn7Xlhim7XPsiOhEIYe5k-X67vo7VMED-1czd-uQ/s640/1%252812%2529.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhVrTsLPtoqzR3H3RlVwJtIWnCbe8pCP2vMh_UeUVfdmb2m3Tdn6vHdO4MKVnNH9zAmcPn5TglLrzi89tieT0411XIUTXpv7XZo66jtn7Xlhim7XPsiOhEIYe5k-X67vo7VMED-1czd-uQ/s72-c/1%252812%2529.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/daraja-la-magara-kuanza-kujengwa-mwezi.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/daraja-la-magara-kuanza-kujengwa-mwezi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy