CCM Z'BAR YATOA MAAGIZO MAZITO KWA JUMUIYA ZAKE

NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR. NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar,  Abdalla Juma Saadala "Mabodi" amezitaka jumuiya za Chama hich...

NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar,  Abdalla Juma Saadala "Mabodi" amezitaka jumuiya za Chama hicho kutumia vizuri fursa ya uchaguzi kuwapitisha viongozi wenye sifa na uwezo wa kukiletea ushindi chama katika Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
Kauli hiyo ameitoa wakati akifungua mafunzo elekezi ya kuwajengea uwezo viongozi wa majimbo Tisa (9) ya Chama na Jumuiya za Mkoa wa Mjini juu ya mabadiliko ya Katiba ya CCM ya 1977 yaliyofanyika hivi karibuni yaliyofanyika Katika ukumbi wa mkoa huo Aman Unguja.
Alisema uchaguzi  unaofanyika hivi sasa katika kwa ngazi mbali mbali za Chama hicho ndio uwanja wa kuandaa jeshi kamili la kisiasa lililokamilika kila idara na lenye ujuzi na mafunzo yote ya vita ya kisiasa litakaloweza kupambana kwa ujasiri na kufanikisha ushindi katika uchaguzi mbali mbali za Dola ili CCM iendelee kushinda na kutawala kupitia utaratibu wa Kidemokrasia.
Aliwasihi washiriki wa mafunzo hayo kutumia vyema mafunzo hayo ya siku moja ili waweze kuwa na uelewa mpana wa Mabadiliko kadhaa yaliyofanyika ndani ya katiba ya CCM ili watekeleze kwa ufanisi majukumu yao na kuwaelimisha wanachama wengine juu ya taaluma hiyo.
Dkt.Mabodi alieleza kwamba matarajio ya taasisi hiyo ya kisiasa ni kuona   kasi ya mabadiliko ya kiutendaji kwa haraka hasa kwa viongozi na watumishi wa Chama na jumuiya zake.
Pia aliongeza kwamba mbali na matarajio hayo mafunzo hayo yatamaliza mizozo na malalamiko yaliyokuwa yalisababisha kutokuwepo kwa ufanisi mzuri wa kiutendaji kwa baadhi ya maeneo ndani ya Mkoa huo.
Naibu Katibu Mkuu huyo alisema hatovumilia tabia za kupangwa safu za viongozi  kwani kufanya hivyo ni kukiuka Kanuni za maadili na miongozo ya uchaguzi huo.
" Tumekuwa tukisema siku zote kuwa CCM ndio mwalimu wa Demokrasia yaani hivyo vyama vya upinzani demokrasia na ustaarabu wa kisiasa tumewafunza sisi hivyo dhana hizo lazima tuzisimamie na kuzitekeleza kwa vitendo kupitia uchaguzi unaoendelea ndani ya taasisi yetu.", alisema Dkt.Mabodi na kuzitaka kamati za uchaguzi na maadili kufuatilia kwa kina mwenendo wa uchaguzi na watakapobaini kasoro watoe taarifa kwa ngazi husika ili zitafutiwe ufumbuzi wa haraka.
Alifafanua kwamba kupitia uchaguzi huo panatakiwa kupatikana viongozi na watendaji watakaoendeleza siasa za upendo, maendeleo, umoja pamoja na mshikamano unaojali misingi ya kidemokrasia ndani na nje ya taasisi hiyo.
Hata hivyo alieleza dhamira ya chama hicho kupitia mabadiliko yaliyofanyika katika Katiba ya Taasisi hiyo kuwa ni pamoja na kila mwanachama kujipanga kisaikolojia kusaidia kuimarisha uchumi wa CCM kupitia rasilimali zilizopo sambamba na kubuni miradi mingine ya kimaendeleo.
Sambamba na hayo kupitia Mafunzo hayo Dkt.Mabodi aliwakumbusha washiriki hao kwamba ili wafanikiwe katika utendaji wao ni lazima watumie vizuri rasilimali watu ya wazee wa CCM pamoja na wastaafu katika sekta za umma na binafsi kwani wana uwezo na uzoefu mkubwa  wa kushauri na kutoa maelekezo mazuri juu ya masuala mbali mbali ya kiutendaji ndani ya Chama hicho.
Mapema akizungumza katika mafunzo hayo Mwenyekiti wa Mkoa huo, Nd. Bora afya Juma Silima alisema Mkoa huo umejipanga kufanikisha kwa ufanisi uchaguzi huo ili kulinda historia ya chama hicho katika kufanikisha uchaguzi unaoheshimu misingi ya utawala bora na demokrasia kwa wananchi wote.

Ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar  Dkt. Abdalla Juma Saadala akizungumza wakati wa mafunzo elekezi ya kuwajengea uwezo watendaji na viongozi wa Majimbo 9 ya CCM na jumuiya zake Mkoa wa Mjini Unguja.
 
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakisikiliza kwa makini Nasaha za Mgeni rasmi  Dkt. Abdalla Juma Saadala huko ktk ukumbi wa Mkoa huo Aman Unguja.

 

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: CCM Z'BAR YATOA MAAGIZO MAZITO KWA JUMUIYA ZAKE
CCM Z'BAR YATOA MAAGIZO MAZITO KWA JUMUIYA ZAKE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhlCtuI-u1Wb3rimDWYhMuan0xqs0ozrUxZQUNL7FNTUlWSyKj6R4nuCKo72giDoQxEX-avd0jsM8Q3Z2URjwvwhtXTxlIhUZbqlRn359p13AcHkoZNhHUDzBxgcvaa8vLQLd8ctBjpbRM/s640/01%25286%2529.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhlCtuI-u1Wb3rimDWYhMuan0xqs0ozrUxZQUNL7FNTUlWSyKj6R4nuCKo72giDoQxEX-avd0jsM8Q3Z2URjwvwhtXTxlIhUZbqlRn359p13AcHkoZNhHUDzBxgcvaa8vLQLd8ctBjpbRM/s72-c/01%25286%2529.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/ccm-zbar-yatoa-maagizo-mazito-kwa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/ccm-zbar-yatoa-maagizo-mazito-kwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy