Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker (kushoto) pamoja na Mkuu wa Idara ya Biashara wa Benki ya NMB, Jam...
BENKI ya
NMB imezindua akaunti mpya kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati
ijulikanayo kama 'NMB FANIKIWA ACCOUNT' ili waweze kukua kibiashara
pamoja na kupata maendeleo ya biashara wanazozifanya.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa
akaunti hiyo ya wafanyabiashara wadogo na wakati, Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki hiyo, Ineke Bussemaker, alisema kuwa akaunti hiyo haina masharti
magumu wakati wa kuifungua pamoja na uendeshaji wake hivyo kuwataka
wafanyabiashara wote kuitumia.
Alisema
kuwa NMB imebuni akaunti hiyo kutokana na kuwepo kwa changamoto ya
wafanyabiashara wadogo kukosa mikopo na kukabiliwa na riba kubwa kwenye
mikopo. Akifafanua zaidi juu ya bidhaa hiyo, Mkuu wa Idara ya Biashara,
James Meitaron alisema Benki ya NMB imeweza kufikia kila kundi katika
kuwanufaisha wafanyabiashara wadogo hasa kimikopo ambapo imewanufaisha
katika kuendeleza biashara zao.
Alisema
Benki ya NMB imekuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na serikali pamoja na
taasisi zake, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha inawakuza wafanyabiashara
wadogo na wakati wakiwemo 'mama lishe'.
COMMENTS