WAZIRI MKUU AKAGUA MAANDALIZI YA SHEREHE ZA MUUNGANO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU    Simu: +255-26-232-2484/232-4560                                         Bar...

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU


  Simu: +255-26-232-2484/232-4560                                       Barabara ya Reli na Mahakama,
Nukushi: +255-26-232-1955,                                         S. L. P. 980,
Barua-pepe: pm@pmo.go.tz                                                       Dodoma,                       
Tovuti:  www.pmo.go.tz                                        Tanzania.


   
24 Aprili, 2017  

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

WAZIRI MKUU AKAGUA MAANDALIZI YA SHEREHE ZA MUUNGANO

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa miundombinu kwa ajili ya sherehe za miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kusema kuwa maandalizi yake yako pazuri.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumatatu, Aprili 24, 2017) mara baada ya kupokea taarifa ya maandalizi na kukagua Uwanja wa Jamhuri ambapo sherehe hizo zitafanyika na uwanja wa Nyerere Square ambako zitafanyika burudani mbalimbali kama sehemu ya maadhimisho hayo.

“Nilikuja kuangalia maandalizi ya sherehe hizo yamefikia wapi, najua kutakuwa na maonyesho ya kijeshi zikiwemo michezo na burudani kutoka Tanzania Bara za Visiwani,” alisema.

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wakazi kutoka wilaya zote za mkoa wa Dodoma na mikoa ya jirani wafike kwenye maonyesho hayo ambayo kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania yanafanyika mkoani humo.

“Tunatarajia wageni wengi kutoka nje ya mkoa huu wakiwemo viongozi wastaafu wa kitaifa, waheshimiwa mabalozi na wake wa waasisi wa Taifa hili, Mama Maria Nyerere na Mama Fatma Karume. Pia tutawatambulisha rasmi ndugu zetu waliochanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964,” alisema.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama alimhakikishia Waziri Mkuu kwamba sehemu zilizobakia zitakamilika kabla ya kesho.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
JUMATATU, APRILI 24, 2017.




COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MKUU AKAGUA MAANDALIZI YA SHEREHE ZA MUUNGANO
WAZIRI MKUU AKAGUA MAANDALIZI YA SHEREHE ZA MUUNGANO
https://lh4.googleusercontent.com/kRgVu1-ttYfCkWwiPC38vk00c2Dz2z9OPsEBA8DRcvRAUk0TS6CRQgC7V7RfualHibbOtSU9gbneWRQJ0fHPtwjkIV0DKhg-eC-JzOk3dfPYWE5ZwhWctfMY9T5Ax8xoG54oiPWmrgfkQ0gePQ
https://lh4.googleusercontent.com/kRgVu1-ttYfCkWwiPC38vk00c2Dz2z9OPsEBA8DRcvRAUk0TS6CRQgC7V7RfualHibbOtSU9gbneWRQJ0fHPtwjkIV0DKhg-eC-JzOk3dfPYWE5ZwhWctfMY9T5Ax8xoG54oiPWmrgfkQ0gePQ=s72-c
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/waziri-mkuu-akagua-maandalizi-ya.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/waziri-mkuu-akagua-maandalizi-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy