Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo akisalimiana na waendesha boda boda, eneo la kwa kwamromboo waliohuduriia kwenye uwekaji w...
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo akisalimiana na waendesha boda boda, eneo la kwa kwamromboo waliohuduriia kwenye uwekaji wa Jiwe la Msingi kwenye Kituo cha Polisi.
1Baadhi wa wananchi waliohudhuria kushuhudia uwekaji wa jiwe la Msingi kwenye Kituo cha Polisi Muriet.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (kwanza kushoto) akiweka Jiwe la Msingi kwenye Ujenzi wa Kituo cha Polisi Muriet.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (kwanza kushoto) akiweka Jiwe la Msingi kwenye Ujenzi wa Kituo cha Polisi Muriet.
Mke wa Mfadhili Bwa.Haroun akivishwa vazi la Kimasai na wakazi wa eneo hilo kama shukrani yao kwa kujengewa Kituo cha Polisi.
Nteghenjwa Hosseah, Arusha
Mkuu
wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo ameweka Jiwe la Msingi
kwenye Kituo cha Polisi Kata ya Muriet wakati wa ziara ya Kikazi Jijini
hapa yenye lengo la kukagua shughuli za maendeleo pamoja na kutatua kero
za wananchi.
Akiweka
jiwe la Msingi Mhe. Gambo amesema kwa muda mrefu alikua anakerwa na
uhalifu uliokithiri katika eneo hilo na hali hiyo kumsukuma yeye
kutafuta mfadhili kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa kituo cha Polisi
kitakachosaidia kudhibiti masuala ya Uhalifu.
Aliongeza
kuwa baada ya kumpata mfadhili huyo alimlete eneo la ujenzi ambapo pia
wahalifu walimuibia Simu yake mbele ya viongozi wa Kamati ya Ulinzi na
Usalama ndipo na mfadhili alipopata ari ya kuanza ujenzi huu haraka
iwezekanavyo.
“Haiwezekani
mtu anaiba mbele ya Kamanda wa Polisi hakika hii ilituthibitishia
kwamba uhalifu katika eneo hili umekithiri na kwa sababu hakunha Kituo
cha Polisi wahalifu wanapata mwanya wa kufanya kazi hii isiyo halali kwa
ujasiri zaidi” Alisema Gambo.
Akizungumza
wakati wa hafla hiyo Mfadhili ambaye ni Mwenyekiti wa Makampuni ya
Lodhia Ndg. Haruni alisema amejitolea sehemu ya mali zake ili kuwasaidia
Watanzania wenzake wanaoteseka na tabia za uhalifu zinazorudisha nyuma
maendeleo
Ujenzi wa Kituo hicho utakaogharimu zaidia ya Tsh Mil 200 utakamilika mnamo mwezi Juni 2017.
COMMENTS