TAHADHARI YATOLEWA KUHUSU DHANA YA ULIPAJI WA KODI YA PANGO LA ARDHI

Mkuu wa kitengo cha Kodi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo  ya Makazi; Dennis Masami akitoa mada kuhusu Maana na Umuhimu wa ulip...




Mkuu wa kitengo cha Kodi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo  ya Makazi; Dennis Masami akitoa mada kuhusu Maana na Umuhimu wa ulipaji Kodi ya pango la Ardhi kwa Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa tahadhari kwa wadaiwa wa kodi ya pango la Ardhi kwa kutoa elimu ya kuhusu dhana ya Kodi hiyo.
Hivi karibuni Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa mafunzo mafupi kwa waandishi wa habari kwa nia ya kuhamasisha ulipaji wa kodi ya pango la Ardhi na kubainisha utofauti wake kati ya kodi hiyo na Kodi ya Majengo ambayo hukusanywa na Mamlaka ya Mapato (TRA).
Akizungumza na waandishi wa habari; Mkuu wa Kitengo cha Kodi; Dennis Masami alisema; Dhana ya ulipaji wa kodi ya pango la Ardhi inatokana na Sheria ya Ardhi namba 4  ya mwaka 1999 katika fungu la 3 kifungu kidogo cha 1 (a) kinachosema: ‘Itambulike kuwa ardhi yote ya Tanzania ni mali ya Umma iliyowekwa chini ya Mheshimiwa Rais kama mdhamini kwa niaba ya wananchi’’
Aliendelea kusema kuwa; Mfumo huu wa umiliki wa ardhi unatambulika kama lease hold na sio free hold, ambapo aina hii ya umiliki ni upangaji katika ardhi, ambao mpangaji anawajibika kufuata masharti ya upangishaji, mojawapo ya masharti hayo ni kulipa pango la kipande cha ardhi. Ambayo Mmiliki ni Rais kwa niaba ya umma na mpangaji ni Mwananchi.
Naye Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mhe. William Lukuvi ametoa tahadhari kwa wasiolipa Kodi ya Pango la Ardhi akisema; “Wale wote ambao hawajalipa Kodi ya Pango la Ardhi, wote wanao miliki  viwanja na mashamba yaliyopimwa, wahusike kulipa kabla ya mwisho wa mwezi wa sita (6). Ifikapo tarehe 30/06 hatua zifuatazo zitachukuliwa dhidi yao; Watashitakiwa Mahakamani, Mali zao zikamatwe na majengo yapigwe mnada kupitia madalali na Miliki zao zifutwe.
Alisema hatua hizo zote zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria, na kutoa tahadhari kuwa kila mmoja achukue hatua ya kulipa kwa hiari kwa Maendeleo ya Taifa.   
(Na kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi)


COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TAHADHARI YATOLEWA KUHUSU DHANA YA ULIPAJI WA KODI YA PANGO LA ARDHI
TAHADHARI YATOLEWA KUHUSU DHANA YA ULIPAJI WA KODI YA PANGO LA ARDHI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjT_j-FVasOQs7j4ueZYu6Iv2Cw93ZHR6WkMYQqOoMmoWbTYmV8I_ryKzt5WIQnJIu7P77tKZYruiZmSlHtHqv-HNmHoEP_PntW2f0HYIxJZuGvK73g7N6T0wCuKMbckVyi9qtUgPYx66I/s640/kodi+ardhi.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjT_j-FVasOQs7j4ueZYu6Iv2Cw93ZHR6WkMYQqOoMmoWbTYmV8I_ryKzt5WIQnJIu7P77tKZYruiZmSlHtHqv-HNmHoEP_PntW2f0HYIxJZuGvK73g7N6T0wCuKMbckVyi9qtUgPYx66I/s72-c/kodi+ardhi.png
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/tahadhari-yatolewa-kuhusu-dhana-ya.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/tahadhari-yatolewa-kuhusu-dhana-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy