Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitakiana amani na mmoja wa mapadre katika Kanisa la Kuu la Katoli...
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitakiana
amani na mmoja wa mapadre katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya
Kristo Mfalme Moshi Mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili 30,
2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
akipokea Ekaristi Takatifu toka kwa Askofu Isaac Aman katika Kanisa la
Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada
ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
akiungana na waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya Kristo
Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili 30, 2017
Waumini
wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John
Pombe Magufuli aliposalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki
Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili
30, 2017
Waumini
wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John
Pombe Magufuli akisalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki
Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili
30, 2017
Waumini
wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John
Pombe Magufuli akisalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki
Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili
30, 2017
Waumini
wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John
Pombe Magufuli aliposalimia waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki
Parokia ya Kristo Mfalme Moshi mjini katika ibada ya Jumapili leo Aprili
30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
akiombewa na Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia
ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili
30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
akiombewa na Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia
ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili
30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
akiombewa na Askofu Isaac Aman katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia
ya Kristo Mfalme Moshi mjini alikohudhuria ibada ya Jumapili leo Aprili
30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
akisalimiana na watawa katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya
Kristo Mfalme Moshi mjini baada ya ibada ya Jumapili leo Aprili 30,
2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
akisalimiana na waumini katika Kanisa la Kuu la Katoliki Parokia ya
Kristo Mfalme Moshi mjini baada ya ibada ya Jumapili leo Aprili 30,
2017
Askofu
Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo akitoa mahubiri wakati wa ibada
ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika
wa Moshi Mjini leo Aprili 30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na
waumini wengine wakimsikiliza Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick
Shoo akitoa mahubiri wakati wa ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT
Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo Aprili 30,
2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akikaribishwa na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo kuongea
na wananchi baada ya ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi
ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo Aprili 30, 2017
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akikaribishwa na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo kuongea
na wananchi baada ya ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi
ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo Aprili 30, 2017
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea
na waumini na wananchi baada ya ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT
Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo Aprili 30,
2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiongea na waumini na wananchi baada ya ibada ya Jumapili katika
Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo
Aprili 30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiombewa sala maalumu na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick
Shoo kuongea na wananchi baada ya ibada ya Jumapili katika Kanisa la
KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo Aprili
30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na
Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo pamoja na Mkuu wa Mkoa wa
Dar es salaam Mhe. Said Meck Sadick wakati wa kuhitimisha ibada ya
Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa
Moshi Mjini leo Aprili 30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiongozana na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo baada ya
ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika
Usharika wa Moshi Mjini leo Aprili 30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli,
Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo, Waziri Ofisi ya Waziri
Mkuu (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista
Muhagama, Askofu Mstaafu Evarist Kweka wakipata picha ya pamoja baada
ya ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika
Usharika wa Moshi Mjini leo Aprili 30, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiongea na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo na Askofu
Mstaafu Evarist Kweka baada ya ibada ya Jumapili katika Kanisa la KKKT
Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi Mjini leo Aprili 30,
2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiongea na Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo na Askofu
Mstaafu Evarist Kweka na kiongozi mwingine baada ya ibada ya Jumapili
katika Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini katika Usharika wa Moshi
Mjini leo Aprili 30, 2017. (PICHA NA IKULU)
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi: 255-22-2113425 |
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 30 Aprili 2017, ameungana na waumini wa dini ya Kikristo kusali ibada ya Jumapili katika Kanisa la Kiaskofu, Jimbo Katoliki la Moshi ,Parokia ya Kristo Mfalme na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Moshi Mjini, Dayosisi ya Kaskazini mkoani Kilimanjaro na kuwataka waumini wa makanisa hayo na Watanzania kwa ujumla kuendeleza amani iliyopo nchini kwa kuwa ndio chachu ya Maendeleo.
Rais Magufuli amesema hatua zinazochukuliwa na Serikali ya awamu ya Tano zina lengo la kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli ya taifa linalomuamini MUNGU.
'' Napenda muniamini kuwa mimi nipo kwa niaba yenu, najua huu Urais si wangu, Urais mnao ninyi mlioamuwa nitumike kama mtumishi kwa wakati huu, nawaomba sana muendelee kuniweka katika sala zenu ili kazi hii ya Urais isinipe kiburi, nikawe mtumishi wa watu'' Amesema Rais Magufuli.
Rais Magufuli amewashukuru waumini wa makanisa hayo mawili na watanzania kwa ujumla kwa kusimama pamoja kuliombea Taifa amani iliyowezesha wananchi kupiga kura kwa amani katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na kutokana na sala zao Mwenyezi MUNGU akamuwezesha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha, Rais Magufuli ametoa msaada wa mifuko 100 ya Saruji kusaidia maendeleo ya kanisa Katoliki na Shilingi Milioni Moja kwa Kwaya ya Kanisa hilo ili irekodi nyimbo zake, halikadhalka katika Kanisa la KKKT, Mheshimiwa Rais ametoa mifuko 150 ya Saruji kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya Kanisa hilo na Shilingi milioni Moja kwa Kwaya ya Kanisa hilo.
Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Mhagama amemuunga mkono Rais Magufuli kwa Kuchangia Mifuko hamsini ya Saruji ambapo Mkuu wa Mkoa wa kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick amechangia mifuko hamsini ya Saruji na Shilingi laki Tano.
Kwa upande wake Askofu wa Jimbo Katoliki la Moshi ,Parokia ya Kristo Mfalme Askofu Isaac Amani amemshukuru Rais Magufuli kwa uwamuzi wa kusali kanisani hapo na kuwataka waumini wa kanisa hilo na Tanzania kwa ujumla kuendelea kumuombea yeye pamoja na Serikali yake ili iweze kuwatumikia Watanzania katika kuwaletea maendeleo na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya mfano kwa Bara la Afrika.
Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania - KKKT, Askofu Dr Fredrick Shoo amewataka waamini wa kanisa hilo na watanzania kwa ujumla kutokuwa na hofu kwa mambo yanayofanywa na Rais hususani katika kupambana na maovu, dhuluma na ufisadi vikiwemo na badala yake Watanzania wabadilike na kujijengea mazoea ya kufanya kazi halali na kuwa waaminifu na kuwa wazalendo kwa Taifa lao.
Aidha, Askofu Shoo amemuomba Dkt Magufuli kuangalia uwezekano wa kupunguza kodi hususani kwa taasisi za kidini zinzotoa huduma za kijamii zikiwemo zile za Elimu na Afya.
Akijibu Maombi hayo Rais Dkt Magufuli amewaeleza waamini na watanzania kwa ujumla kuwa Serikali inathamini michango ya huduma za kijamii zinazotolewa na Taasisi za dini na kuahidi kuliangalia suala hilo.
Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU.
Moshi, Kilimanjaro.
30 Aprili, 2017.
COMMENTS