NA K-VA BLOG NA MASHIRIKA YA HABARI LILE pambano la watani wa jadi nchini Hispania, (El Clasico), baina ya Real Madrid ...
NA
K-VA BLOG NA MASHIRIKA YA HABARI
LILE
pambano la watani wa jadi nchini Hispania, (El Clasico), baina ya Real Madrid
na Barcelona la ligi kuu ya soka nchi humo maarufu kama Laliga, lilimalizika
usiku wa kuamkia leo Aprili 24, 2017 kwa Barca kushinda mabao 3-2.
Hata
hivyo Barca imeshinda Madridi ikiwa pungufu kufuatia mlinzi wake na nahodha wa
timu hiyo, Sergio Ramos, kutolewa nje ka kadi nyekundu kufuatia rafu
aliyomchezea mshambuliaji hatari wa Barca, Leonel Messi, zikiwa zimesalia si
zaidi ya dakika 20 mpira kumalizika.
Pambano
hilo lililokuwa la marudiano na kuchezwa kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu,
Madrid ilikuwa ya kwanza kujipatia bao katika kipindi cha kwanza kupitia kwa
kiungo wa kati wa timu hiyo Cacemiro, kufuatia mpira wa krosi uliopigwa na
Marcello kutoka wingi ya kushoto.
Hata
hivyo Barca ilisawazisha bao hilo dakika chache kabla ya mpira kwenda mapumziko
kupitia kwa winga wake Ra
BAO
la 500 la Lionel Messi limeipeleka Barcelona kwenye uongozi wa ligi kuu ya
Hispania Laliga katika muda wa majeruhi dhidi ya wachezaji pungufu wa Real
Madrid kwenye uwanja wa ugenini wa Santiago Bernabeu nchini Hispania usiku wa
kuamkia leo Aprili 24, 2017
Ushindi
wa mabao 3-2 wa El Clasico dhidi ya hasimu wake Madrid, unaifanya Barca kuwa na
pointi sawa na Madrid lakini kwa rekodi nzuri ya kukabana koo kileleni.
Casemiro
alifunga bao la kwanza na la kuongoza kabla ya Messi kusawazisha na Ivan
Rakitic kuiweka Barcelona mbele huku Nahodha wa Madrid, Sergio Ramos,
akionyeshwa kadi nyekundu kutokana na kumchezea vibaya Messi.
Kocha
Mkuu wa Madrid, Zenadine Zidane, “Zizu” alifanya mabadiliko kwa kumuingiza
James Rodriguez ambaye alifunga bao la kusawazisha, kabla ya Messi kufunga bao
la ushindi kwenye muda wa majeruhi.
COMMENTS