Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba amekutana na kufanya mazunguzo na Mabaloz...
Naibu
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt.
Susan Kolimba amekutana na kufanya mazunguzo na Mabalozi Wateule
wanaoenda kuiwakilisha Tanzania maeneo mbalimbali Duniani.Mazungumzo
hayo yaliyofanyika ofisini kwake Makao Makuu ya Nchi mjini Dodoma,
yalijikita katika kujadili namna bora ya kuiwakilisha Tanzania ughaibuni
kwa kuzingatia sera ya nchi ya mambo ya nje, kwa lengo la kuboresha
mahusiano ya Kidiplomasia baina ya Tanzania na nchi hizo, na kwa
kuzingatia maslahi mapana ya kiuchumi ya nchi yetu ikiwemo kutangaza
shughuli za utalii zinazopatikana nchini.
Naibu Waziri Mhe. Dkt. Susan Kolimba akisisitiza jambo
Balozi
Mteule Baraka H. Luvanda akichangia jambo wakati wa mazungumzo. Punde
baada ya mazungumzo na Mhe. Naibu Waziri, Mabalozi walikutana na kufanya
mazungumzo na Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki
Katibu
Mkuu Wizara Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi
Dkt.Aziz P Mlima akiongea na Mabalozi ofisini kwake mjini Dodoma
Mazunguzo yakiendelea
COMMENTS