Kikosi cha Kitaifa cha kunusuru Ikolojia ya Mto Ruaha kilichoundwa na Makamu wa Rais wa Tanzania kilichoko Mkoani Mbeya, kimeeendel...
Kikosi cha Kitaifa cha kunusuru Ikolojia ya Mto Ruaha kilichoundwa na Makamu wa Rais wa Tanzania kilichoko Mkoani Mbeya, kimeeendelea na ziara yake kwa kutembelea skimu ya Mwendamtitu iliyopo wilayani Mbarali. Katika ziara hiyo Kikosi kazi kiligundua jinsi ambavyo miundombinu ya skimu hiyo inavyopoteza maji ambayo yalitakiwa kuingia Mto Ruaha.
Aidha
pia kimegundua kuwa skimu hiyo imeanzishwa pasipo kufuata sheria za
umwagiliaji kwani haina kibali cha umwagiliaji wala kibali cha matumizi
ya maji yanayoingia katika mfereji wa skimu hiyo.
Wakiongea
katika ziara hiyo Wajumbe wamesikitishwa an kitendo cha skimu hiyo cha
kutumia maji mengi pasipo kuwa na kibali chochote wala pasipo kuwa na
miundombinu ya mifereji inayowezesha maji kurudi mto Ruaha mKuu.” Katika
skimu hii Maji yanatitririka bure na kwa aina hii ya umwagiliaji kamwe
mto Ruaha Mkuu hautapata maji, ila tutachukua hatua stahiki” aliongea
Mjumbe Injinia Seth Luswema.
Kwa
upande wa wananchi wa eneo hilo wameiomba Serikali iwasaidie kuwapatia
elimu jinsi ya kuendesha skimu hiyo na pia kuelekezwa jinsi ya kuweka
miundombinu rafiki kwa ajili ya kuokoa kiasi cha maji kinachopotea.
Wamesema wao hawana elimu yoyote na hawajui kama wanakosea kwa jinsi
wanavyoendesha skimu hiyo.
Kikosi
hiko bado kipo Mkoani Mbeaya katika wilaya ya Mbalari kwa ajili y
akuzungukia na kukagua maeneo mbalimbali amabayo yanachangia maji
kutokwenda Mto Ruaha Mkuu.
Mjumbe
wa Kikosi kazi Injinia Seth Luswema (wa kwanza kushoto), akiwa meza kuu
pamoja na Viongozi wa Chama kwa wilaya ya Mbalari, Kuanzia kushoto ni
Mwenyekiti wa kamati ya Ujenzi, uchumi na maliasili, Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, Katibu wa CCM wilaya na Mwenyekiti wa
CCM wa Wilaya ya Mbalari.
Wajumbe
wa Kikosi kazi cha Kitaifa cha kunusuru ikolojia ya mto Ruaha, wakipata
maelekezo toka kwa Katibu wa skimu ya umwagiliaji ya Mwendomtitu
akielekeza juu ya wanavyotumia maji ya umwagiliaji ya Mto Ruaha
kumwagilizia mashamba ya mpunga.
shamba
la vitunguu lililoko karibu na kianziao cha maji cha askimu cha
mwendamtitu wilayani Mbalari likionekana kushamiri kwa sabau ya maji ya
kusukuma na pampu wanayotoa mto Ruaha.
Wajumbe wa Kikosi kazi wakisikiliza maoni ya Wananchi wa kata ya Mwendamtitu walipotembelea skimu yao ya umwagiliaji.
COMMENTS