KARIAKOO FAMILY DEVELOPMENT FOUNDATION CHAPATA UONGOZI MPYA

Wanachama wa chama cha  Kariakoo Family Development Foundation (KFDF) wamejipatia uongozi mpya baada ya kufanya mkutano mkuu wa uchaguzi s...


Wanachama wa chama cha  Kariakoo Family Development Foundation (KFDF) wamejipatia uongozi mpya baada ya kufanya mkutano mkuu wa uchaguzi siku ya Jumapili Aprili 23, 2017 katika ukumbi wa shule ya Msingi ya Jamhuri jijini Dar es salaam. Jumla ya wanachama hai na halali  41 walishirki katika uchaguzi huo, ambapo wanachama 23 walikuwepo ukumbini na wanachama 18 waishio nje ya nchi walipiga kura kwa njia ya mtandao. 
Bw. Alkarim Bhanji alishinda nafasi ya Uenyekiti akiwa mgombea pekee, wakati Bw. Mohamed Irapo alinyakua nafasi ya Makamu Mwenyekiti. Katibu Mkuu wa kipindi cha mpito Bw. Wahid Abdulghafoor aliweza kutetea kiti chake akiwa mgombea pekee. Nafasi ya Katibu Mkuu msaidizi imechukuliwa na Bw. Fabian Kimongw wakati Bw. Bakari Simba ametetea tena nafasi ya Mweka Hazina Msaidizi aliyokuwa akishika wakati wa kipindi cha mpito.
Katika uchaguzi huo uliokuwa umesimamiwa vyema na Katibu Mkuu wa klabu ya michezo ya Saigon,  Bw. Boi Juma,  jumla ya wajumbe watano kati ya sita wanaotakiwa kikatiba walichaguliwa. Hao ni  Bw. Shaaban Kessy Mtambo,  Bw. Abdallah Kizua,  Bw. Idrissa Jumbe, Bi. Sophia Muccadam na Bi. Salma King.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa KFDF Bw. Wahid Abdulghafoor, nafasi mbili za Mweka Hazina na Mjumbe mmoja zilizo wazi baada ya kutotokea mgombea zitajazwa baadaye katika uchaguzi mdogo.

KFDF ni chama kinachojumuisha wananchi  wanaoishi  ama waliopata kuishi eneo lote Kariakoo, dhumuni kuu likiwa ni kuwaunganisha upya na kufanya shughuli za kijamii kimaendeleo kwa lengo la kudumisha na kuendeleza umoja, mshikamano na undugu uliokuwepo miongoni mwa wakaazi wa eneo hilo maarufu la jiji la Dar es salaam toka enzi za mababu.


Msimamizi wa uchaguzi Bw. Boi Juma (mwenye bahasha mkononi) akipata picha ya pamoja na safu mpya ya uongozi wa KFDF pamoja na wanachama waliopo nchini baada ya kuhitimisha zoezi hilo siku ya Jumapili Aprili 23, 2017 katika ukumbi wa shule ya Msingi ya Jamhuri jijini Dar es salaam


Msimamizi wa uchaguzi Bw. Boi Juma (kati) akipata picha ya pamoja na safu mpya ya uongozi wa KFDF siku ya Jumapili Aprili 23, 2017 katika ukumbi wa shule ya Msingi ya Jamhuri jijini Dar es salaam.
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KARIAKOO FAMILY DEVELOPMENT FOUNDATION CHAPATA UONGOZI MPYA
KARIAKOO FAMILY DEVELOPMENT FOUNDATION CHAPATA UONGOZI MPYA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhaIZFyr3r2ABYSIvDpb912UPJYUijZDgs6f7kPobKEsEzOpmxpaPE9wYghyphenhyphenzRftN5Fv4YtzsJ1mUeB1u_kbgvuzZRw6kqPLVEAdZfEBF0tD2rsdSfC4KKGFBqalDS1zY7hceD2HmMxMoY/s640/IMG_1029.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhaIZFyr3r2ABYSIvDpb912UPJYUijZDgs6f7kPobKEsEzOpmxpaPE9wYghyphenhyphenzRftN5Fv4YtzsJ1mUeB1u_kbgvuzZRw6kqPLVEAdZfEBF0tD2rsdSfC4KKGFBqalDS1zY7hceD2HmMxMoY/s72-c/IMG_1029.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/kariakoo-family-development-foundation.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/04/kariakoo-family-development-foundation.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy