Baadhi ya wafanyakazi wanawake wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakifurahia wakati wa kusherehekea siku ya Wanawake Duniani kwenye viwanja...
Baadhi ya wafanyakazi wanawake wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakifurahia wakati wa kusherehekea siku ya Wanawake Duniani kwenye viwanja vya Mwembe-Yanga wilayani Temeke jijini Dar es Salaam, Machi 8, 2018.
Baadhi ya wafanyakazi wanawake wa Mfuko wa Pensheni
wa PPF, wakipita mbele ya jukwaa kuu wakati wa kusherehekea siku ya Wanawake Duniani kwenye viwanja vya Mwembe-Yanga wilayani Temeke jijini Dar es Salaam, Machi 8, 2018.
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
WAFANYAKAZI Wanawake wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, leo Machi 8, 2017, wameungana na wenzao katika kusherehekea siku ya Wanawake Duniani kwenye viwanja vya Mwembe- Yanga
jijini Dar es Salaam.
jijini Dar es Salaam.
Katika maadhimisho hayo yaliyohanikizwa na mvua za rasharasha, wanawake hao wakiwa na furaha, walipita mbele ya viongozi wakuu wa mkoa na kuonhyesha mabango yao
yaliyokuwa na ujumbe tofauti tofauti.
yaliyokuwa na ujumbe tofauti tofauti.
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu isemayo “Tanzania
ya viwanda, Wanawake ndio Msingi wa Mabadiliko ya Kiuchumi”.
ya viwanda, Wanawake ndio Msingi wa Mabadiliko ya Kiuchumi”.
Kauli mbiu hiyo inalenga kuikumbusha jamii kuhusu umuhimu wa kujenga mazingira wezeshi kwa Wanawake hasa kutambua mchango wao katika kuleta Maendeleo yao na
ya jamii kwa ujumla.
ya jamii kwa ujumla.
Katika maadhimisho hayo ya siku ya Wanawake Duniani Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaviva, ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, ambaye awali Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,
ilisema Mkuu huyo wa Mkoa ndiye angekuwa mgeni rasmi lakini hakutokea.
ilisema Mkuu huyo wa Mkoa ndiye angekuwa mgeni rasmi lakini hakutokea.
Katika hotuba yake, Mkuu wa Wilaya ya Temeke, alisema jamii inapaswa kutimiza wajibu wake ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha, kuwaamini na kuwapa Wanawake haki sawa katika nafasi za Elimu, Uchumi na uongozi ili wawe chachu ya mabadiliko yenye lengo la kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
Baadhi ya akina mama wa taasisi ya THTU nao wakipita mbele ya jukwa kuu
Baadhi ya wafanyakazi wanawake wa Mfuko wa Pensheni
wa PPF, wakipita mbele ya jukwaa kuu wakati wa kusherehekea siku ya Wanawake Duniani kwenye viwanja vya Mwembe-Yanga wilayani Temeke jijini Dar es Salaam, Machi 8, 2018.
Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, Felix Lyaviva, (kushoto), akiteta jambo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando, wakati wakipokea maandamano ya akina mama. Lyaviva alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Baadhi ya wanawake wa TANESCO nao wakipita mbele ya jukwaa kuu
Mwanadada mwenye kipaji cha kusakata kabumbu akionyesha umahiri wake, hii ilikuwa ni sehemu ya burudani zilizokuwepo uwanjani
Picha ya pamoja ikionyesha wafanyakazi wanawake ya PPF walioshiriki kwenye maadhimisho hayo.
COMMENTS