TUNDU LISSU AFUTIWA MASHTAKA YA UCHOCHEZI NA KUKAMATWA TENA NA POLISI

Tundu Lissu, akiw...


Tundu Lissu, akiwa ameketi sanjari na polisi wa mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, Machi 7, 2017 muda mfupi kabla ya kufutiwa mashtaka na serikali na kukamatwa tena na polisi.
 
MWANASHERIA Mkuu wa CHADEMA, ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, amefutiwa mashtaka ya uchochezi, baada ya Ofisi ya mashtaka ya serikali kuieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, Machi 6, 2017 kuwa haina haja ya kuendelea na kesi hiyo ya uchochezi.
Hata hivyo Mwanasheria huyo machachari, alikamatwa hata kabla ya kuondoka kwenye mahakama hiyo na sasa anashikiliwa kwenye kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam.
Habari za kukamatwa kwake amethibitisha Tundu Lissu mwenyewe  kwenye ukurasa wake wa Facebook, akiuarifu umma wa Watanzania.
“Nimekamatwa tena hapa hapa mahakamani Kisutu mara tu baada ya waendesha mashtaka wa serikali kunifutia kesi iliyotokana na kukamatwa kwangu bungeni Dodoma mwezi uliopita.”. Ameandika Tundu Lissu.
Amesema serikali imeifuta kesi hiyo kwa maelezo kwamba haina nia tena ya kuendelea na kesi hiyo. “Sikutoka hata nje ya mahakama nikakamatwa tena. Wamenileta Central kwa mahojiano. Mapolisi walionikamata wamekataa kuniambia wananikamata kwa kosa gani.” Ameendelea kuandika Tundu Lissu ambaye anagombea Urais kwenye uchaguzi Mkuu wa chama cha Wanasheria Tanzania, (TLS), utakaofanyika wiki ijayo jijini Arusha.
Tundu Lissu katika maelezo yake amesema “Nadhani sababu ina uhusiano wa moja kwa moja na Uchaguzi wa Rais wa TLS unaofanyika wiki ijayo. Serikali hii, kwa kutumia mawakili wao, imekuwa na mkakati mkubwa wa kunizuia kugombea urais wa TLS.” Amesema Mwanasheria huyo.
 

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TUNDU LISSU AFUTIWA MASHTAKA YA UCHOCHEZI NA KUKAMATWA TENA NA POLISI
TUNDU LISSU AFUTIWA MASHTAKA YA UCHOCHEZI NA KUKAMATWA TENA NA POLISI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiFslQVq0E5A9BhTL3UZouRme52ZmVQ5kcnHVz2hg2TUqFgKevKa2GatT_mCpWPa09KQvpcW7ecQlqjBl0swo7Khht-pP755j3WL1oRUSZJZ15ZwNem90aE2QuFBUCg5aEcZ8wy5n93XaU/s640/LISSU.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiFslQVq0E5A9BhTL3UZouRme52ZmVQ5kcnHVz2hg2TUqFgKevKa2GatT_mCpWPa09KQvpcW7ecQlqjBl0swo7Khht-pP755j3WL1oRUSZJZ15ZwNem90aE2QuFBUCg5aEcZ8wy5n93XaU/s72-c/LISSU.jpeg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/tundu-lissu-afutiwa-mashtaka-ya.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/tundu-lissu-afutiwa-mashtaka-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy