SINGIDA TUMEFIKISHA MADAKTARI BINGWA KWA WANANCHI NA ZOEZI HILO NI ENDELEVU; DKT NCHIMBI.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akitoa mchango wa fedha kwa ajili ya upasuaji wa macho kwa mgonjwa aliyekosa fedh...


Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akitoa mchango wa fedha kwa ajili ya upasuaji wa macho kwa mgonjwa aliyekosa fedha kiasi cha shilingi elfu thelathini kwa ajili ya huduma za kibingwa Wilayani Mkalama.
 
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na wananchi waliojitokeza kupata hududma za kibingwa katika hospitali ya Iambi ya Wilayani Mkalama.
 
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akipanda Mkorosho katika shamba la Mkulima wa kijiji cha Gumanga wilayani Mkalama kama hamasa kwa wananchi wengine wapande zao hilo.
 
Wananchi wa kijiji cha Nkungi na watendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wakisaidiana kupanda viazi lishe katika shamba la Mkulima ili kuhamasisha kilimo hicho.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ameagiza Kliniki tembezi ya huduma za kibingwa kwa mkoa wa Singida kuwa endelevu huku akizielekeza halmashauri kuandaa mpango wa utekelezaji wa zoezi hilo kwakuwa linagusa maisha ya wananchi wa hali ya chini.

Dokta Nchimbi ametoa agizo hilo mara baada ya kufanya ziara katika Hospitali ya Iambi Wilayani Mkalama ambako zoezi la kliniki tembezi ya madaktari bingwa wa fani nane kwa Mkoa wa Singida lilikuwa linahitimishwa.

Amesema mara baada ya kukamilika kwa halmshauri zote saba mpango wa kuanza kutoa huduma za kibingwa kwa awamu ya pili uanze mara moja kwakuwa wagonjwa wengi walionufaika ni wale webnye kipato duni na walikuwa wameshakata tama ya kupata matibabu.

Dokta Nchimbi ametembelea wodi ya wanawake waliofanyiwa upasuaji na daktari bingwa wa wanawake, wodi ya akina baba waliofanyiwa upasuaji wa magonjwa ya tezi dume na matatizo ya njia ya mkopo pamoja, ametembelea chumba cha upasuaji wagonjwa wa macho na kumalizia wodi ya watoto waliofanyiwa upasuaji kutokana na matatizo ya mfumo wa upumuaji na midomo sungura.

Amesema, “Ukisikiliza ushuhuda wa wagonjwa waliopatiwa matibabu ya kibingwa utaona umuhimu wa kliniki tembezi, wengine walikwisha kata tamaa ya kuishi na kusubiria kifo, wengine walitengwa na kusimangwa, kuna mmoja wakati analetwa hospitali kuonana na madaktari hawa majirani waliwaambia ndugu zake watarudisha maiti lakini amepona kabisa”.

Akitoa taarifa ya kliniki tembezi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dokta John Mwombeki amesema wagonjwa walioonwa na madaktari bingwa kwa muda wa siku nne ni 675 na waliofanyiwa upasuaji ni 71.

Dokta Mwombeki ameeleza kuwa kliniki tembezi imekuwa na manufaa kutokana na kuwa na gharama nafuu kuliko hospitali kubwa za rufaa ambapo wagonjwa wengi wameshindwa kufika huko.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Injinia Geofrey Sanga ameeleza kuwa halmashauri yake imetoa milioni 18 kufanikisha zoezi hilo na kuahidi kuendelea kushikiana na Mkoa katika awamu ya pili ili wananchi wote wenye uhitaji wa huduma za madaktai bingwa wazipate.

Madaktari bingwa wa magonjwa ya ndani, madaktari bingwa wanawake, wototo, macho, upasuaji, mifupa na njia ya mkojo wametoa huduma za kibingwa wilayani Mkalama kuanzia Februari 27 hadi Machi 3.

Wakati huohuo Mkuu wa Mkoa wa Singida amezindua rasmi kilimo cha korosho kwa kushiriki zoezi la upandaji wa mikorosho na mihogo na kuhamasisha wananchi kupanda mikorosho hasa katika mashamba yao waliyolima mihogo.

Dokta Nchimbi amesema korosho ni zao linaloweza kuvunwa kwa zaidi ya miaka hamsini na pia ni rafiki wa mazingira, huku akiendelea kusisitiza kilimo cha viazi lishe kwakuwa ni mkombozi wa uchumi wa wananchi wa Singida.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SINGIDA TUMEFIKISHA MADAKTARI BINGWA KWA WANANCHI NA ZOEZI HILO NI ENDELEVU; DKT NCHIMBI.
SINGIDA TUMEFIKISHA MADAKTARI BINGWA KWA WANANCHI NA ZOEZI HILO NI ENDELEVU; DKT NCHIMBI.
https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEg3Axf2sdRQMVFErpI-QpUCOQTo3T80UA6bfZAFGdsbnI1bs0a93TeM24aEhzMZdnL7el-0OwNSlJEIP0glEtH410jT2pLbYSkmEmvUD4JO0l5DhOkbjn8aP2Ty9eROD68SMNItaJ177nTcfgqqjr_Qu64gAfs7n_7T2i04bDjuYSrHgA=s0-d
https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEg3Axf2sdRQMVFErpI-QpUCOQTo3T80UA6bfZAFGdsbnI1bs0a93TeM24aEhzMZdnL7el-0OwNSlJEIP0glEtH410jT2pLbYSkmEmvUD4JO0l5DhOkbjn8aP2Ty9eROD68SMNItaJ177nTcfgqqjr_Qu64gAfs7n_7T2i04bDjuYSrHgA=s72-c-d
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/singida-tumefikisha-madaktari-bingwa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/singida-tumefikisha-madaktari-bingwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy