Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akitoa mchango wa fedha kwa ajili ya upasuaji wa macho kwa mgonjwa aliyekosa fedh...
Mkuu wa
Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akitoa mchango wa fedha kwa ajili
ya upasuaji wa macho kwa mgonjwa aliyekosa fedha kiasi cha shilingi elfu
thelathini kwa ajili ya huduma za kibingwa Wilayani Mkalama.
Mkuu wa
Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na wananchi
waliojitokeza kupata hududma za kibingwa katika hospitali ya Iambi ya
Wilayani Mkalama.
Mkuu wa
Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akipanda Mkorosho katika shamba la
Mkulima wa kijiji cha Gumanga wilayani Mkalama kama hamasa kwa wananchi
wengine wapande zao hilo.
Wananchi
wa kijiji cha Nkungi na watendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Mkalama
wakisaidiana kupanda viazi lishe katika shamba la Mkulima ili
kuhamasisha kilimo hicho.
Mkuu wa
Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ameagiza Kliniki tembezi ya huduma
za kibingwa kwa mkoa wa Singida kuwa endelevu huku akizielekeza
halmashauri kuandaa mpango wa utekelezaji wa zoezi hilo kwakuwa linagusa
maisha ya wananchi wa hali ya chini.
Dokta
Nchimbi ametoa agizo hilo mara baada ya kufanya ziara katika Hospitali
ya Iambi Wilayani Mkalama ambako zoezi la kliniki tembezi ya madaktari
bingwa wa fani nane kwa Mkoa wa Singida lilikuwa linahitimishwa.
Amesema
mara baada ya kukamilika kwa halmshauri zote saba mpango wa kuanza kutoa
huduma za kibingwa kwa awamu ya pili uanze mara moja kwakuwa wagonjwa
wengi walionufaika ni wale webnye kipato duni na walikuwa wameshakata
tama ya kupata matibabu.
Dokta
Nchimbi ametembelea wodi ya wanawake waliofanyiwa upasuaji na daktari
bingwa wa wanawake, wodi ya akina baba waliofanyiwa upasuaji wa magonjwa
ya tezi dume na matatizo ya njia ya mkopo pamoja, ametembelea chumba
cha upasuaji wagonjwa wa macho na kumalizia wodi ya watoto waliofanyiwa
upasuaji kutokana na matatizo ya mfumo wa upumuaji na midomo sungura.
Amesema,
“Ukisikiliza ushuhuda wa wagonjwa waliopatiwa matibabu ya kibingwa
utaona umuhimu wa kliniki tembezi, wengine walikwisha kata tamaa ya
kuishi na kusubiria kifo, wengine walitengwa na kusimangwa, kuna mmoja
wakati analetwa hospitali kuonana na madaktari hawa majirani waliwaambia
ndugu zake watarudisha maiti lakini amepona kabisa”.
Akitoa
taarifa ya kliniki tembezi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mganga
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dokta John Mwombeki amesema wagonjwa walioonwa
na madaktari bingwa kwa muda wa siku nne ni 675 na waliofanyiwa upasuaji
ni 71.
Dokta
Mwombeki ameeleza kuwa kliniki tembezi imekuwa na manufaa kutokana na
kuwa na gharama nafuu kuliko hospitali kubwa za rufaa ambapo wagonjwa
wengi wameshindwa kufika huko.
Naye
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Injinia Geofrey Sanga
ameeleza kuwa halmashauri yake imetoa milioni 18 kufanikisha zoezi hilo
na kuahidi kuendelea kushikiana na Mkoa katika awamu ya pili ili
wananchi wote wenye uhitaji wa huduma za madaktai bingwa wazipate.
Madaktari
bingwa wa magonjwa ya ndani, madaktari bingwa wanawake, wototo, macho,
upasuaji, mifupa na njia ya mkojo wametoa huduma za kibingwa wilayani
Mkalama kuanzia Februari 27 hadi Machi 3.
Wakati
huohuo Mkuu wa Mkoa wa Singida amezindua rasmi kilimo cha korosho kwa
kushiriki zoezi la upandaji wa mikorosho na mihogo na kuhamasisha
wananchi kupanda mikorosho hasa katika mashamba yao waliyolima mihogo.
Dokta
Nchimbi amesema korosho ni zao linaloweza kuvunwa kwa zaidi ya miaka
hamsini na pia ni rafiki wa mazingira, huku akiendelea kusisitiza kilimo
cha viazi lishe kwakuwa ni mkombozi wa uchumi wa wananchi wa Singida.
COMMENTS