Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akivuta kitambaa pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawas...
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akivuta
kitambaa pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa
Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego kuashiria uwekaji
wa jiwe la msingi katika Ujenzi wa Gati namba mbili litakayojengwa
katika Bandari ya Mtwara.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia
kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Gati namba 2 katika
Bandari ya Mtwara.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa
maelekezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari
Tanzania Mhandisi Deusdedit Kakoko kuhusu eneo ambalo Bandari ya Mtwara
walikuwa wakilihitaji kutoka sehemu nyingine.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania Mhandisi Deusdedit
Kakoko kuhusu eneo ambalo Bandari ya Mtwara walikuwa wakilihitaji kutoka
sehemu nyingine.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka
saini katika kitabu cha wageni kabla ya kuweka jiwe la msingi katika
ujenzi wa Gati namba 2 litakalojengwa katika bandari ya Mtwara.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Mbunge wa Newala George Huruma Mkuchika mara baada ya
kuwasili katika eneo la Bandari ya Mtwara.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango Mtkurugenzi Mkuu wa Benki
ya NMB Ineke Bussemaker wakikata utepe kuashiaria ufunguzi rasmi wa
Kituo cha Biashara cha Benki hiyo mkoani Mtwara
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango Mkurugenzi Mkuu wa Benki
ya NMB Ineke Bussemaker, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego wakipiga
makofi mara baada ya kufungua kituo hicho cha Kibiashara cha NMB mkoani
Mtwara.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NMB Ineke Bussemaker mara baada ya
kukifungua kituo hicho cha kibiashara mkoani Mtwara.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
jambo na Mbunge wa Mtwara mjini kupitia Chama cha Wananchi (CUF) Maftah
Nachuma mara baada ya kufungua kituo hicho cha kibiashara cha Benki ya
NMB mkoani Mtwara.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa
maelekezo kwa Mbunge wa Mtama Nape Nnauye kuhusu ujenzi wa Kituo cha
Afya cha Mnolela ambapo pia amechangia kiasi cha Shilingi milioni 15 na
akamuagiza Mbunge huyo kuchangia Shilingi milioni 10 kutoka fedha za
jimbo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia
katika kijiji cha Madangwa katika jimbo la Mtama mkoani Lindi.
Mjumbe
wa Halmashauri kuu ya CCM na Mbunge mteule wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete akifUatilia hotuba ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati
aliposimamishwa njiani na Wanakijiji wa Madangwa katika jimbo la Mtama
mkoani Lindi. (PICHA NA IKULU)
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Faksi: 255-22-2113425 |
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli,
ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kuachana na
utaratibu wa kutoa zabuni za uendeshaji wa bandari kwa kampuni binafsi
ambazo huingia mikataba isiyo na manufaa kwa nchi na kusababisha uwepo
mianya ya upotevu wa fedha za umma.
Mhe.
Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 04 Machi, 2017 muda mfupi
kabla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa gati namba 2 ya bandari ya
Mtwara ambayo ujenzi wake unatarajiwa kuchukua muda wa miezi 21 kuanzia
sasa.
"Kwa
sababu mmeamua kuichimba hii bandari ili kuongeza kina mpaka mita 15
kwa kutumia fedha zetu, sitegemei TPA na Wizara kuingia tena mkataba na
wawekezaji wengine, kwa sababu imekuwa ni kawaida hapa Tanzania,
tunatumia fedha zetu halafu wanakuja watu wengine kufanya biashara na
fedha zetu kana kwamba nchi hii haina wasomi, na wanaokuja kuendesha
kweli wanaiba" amesema Mhe. Rais Magufuli.
Mapema
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema
gati namba 2 itakayojengwa katika bandari ya Mtwara itakuwa na urefu wa
mita 350 na ujenzi wake utagharimu Shilingi Bilioni 137.5 zote zikiwa
zimetolewa na Serikali ya Tanzania.
Nae
Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mhandisi Deusdedit Kakoko amesema imelazimu
kuongeza gati katika bandari ya Mtwara baada ya kuwepo ongezeko la
mizigo inayosafirishwa kupitia bandari hiyo ambapo kiwango cha mizigo
inayohudumiwa kinatarajiwa kuongezeka kutoka tani 273,886 mwaka
2015/2016 hadi kufikia tani 388,000 mwaka 2016/2017 kiwango ambacho
kinakaribia ukomo wa uwezo wa bandari hiyo yenye uwezo wa kuhudumia tani
400,000 kwa mwaka.
Wakati huo huo, Mhe.
Rais Magufuli amefungua Kituo cha Biashara cha Benki ya NMB Mjini
Mtwara na kutoa maagizo kwa Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip
Mpango kutoa maelekezo ili fedha zote za Serikali zipitie Benki ya NMB
ambayo licha ya hisa zake kumilikiwa na Serikali kwa asilimia 32 imekuwa
ikitoa gawio kwa Serikali kila mwaka ambapo mwaka 2016 ilitoa Shilingi
Bilioni 16.5 na mwaka huu inatarajia kutoa zaidi ya kiwango hicho cha
gawio.
"Na
nikuombe Waziri, kwa sababu wewe ndio unayesimamia fedha za Serikali,
toa maelekezo ili fedha zote zipitie benki ya NMB, labda kama kutakuwa
na umuhimu sana wa kupitia benki nyingine" amesema Mhe. Rais Magufuli.
Mhe.
Rais Magufuli ambaye ameipongeza benki ya NMB kwa kujikita kutoa huduma
za kibenki kwa wananchi wa kawaida na wafanyakazi nchi nzima ametoa
wito kwa benki zote nchi kupunguza viwango vya riba ili Watanzania wengi
waweze kukopa na kufanya shughuli za uzalishaji mali.
Katika hatua nyingine,
Mhe. Rais Magufuli amefungua jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Mjini
Mtwara ambalo limejengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 31 na linatoa
huduma za Benki Kuu katika kanda ya kusini inayojumuisha Mikoa ya
Mtwara, Lindi na sehemu za Mikoa ya Pwani na Ruvuma.
Pamoja
na kumpongeza Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete
kwa kuridhia ujenzi wa jengo hilo na kuipongeza BOT kwa kufanikisha
ujenzi huo na kusimamia vizuri uchumi wa nchi, Mhe. Rais Magufuli
ameitaka benki hiyo kuu kuchukua hatua kali dhidi ya benki ambazo
zimekuwa zikikiuka maadili na taratibu za kibenki ikiwemo kushiriki
njama za kuiba fedha za Serikali kupitia mikopo na utakatishaji wa
fedha.
Aidha,
amemtaka Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Benno Ndulu aandae
utaratibu utakaozibana benki zinazofanya biashara hapa nchini ili
zilazimike kuwakopesha wananchi, kupunguza viwango vya riba na
kuendeleza shughuli za uzalishaji mali.
Mhe.
Rais Magufuli pia amefungua nyumba 40 za makazi za Rahaleo zilizojengwa
na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mjini Mtwara kwa gharama ya
Shilingi Bilioni 10.5 na ameipongeza NHC kwa kazi nzuri ya ujenzi wa
nyumba za makazi ya wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.
Akiwa
katika mradi huu Mhe. Dkt. Magufuli ameagiza kuanzia sasa Mkoa, Wilaya
ama Kiongozi yeyote atakayeomba kujengewa makazi na NHC ahakikishe eneo
lililoandaliwa kwa ajili ya kujengwa makazi hayo linafikishiwa barabara,
umeme na maji na ameitaka NHC kuacha kutumia wakandarasi katika ujenzi
wa majengo yake na badala yake waunde vikosi kazi vya ujenzi kwa kutumia
wataalamu waliopo ndani ya nchi ili kuzalisha ajira zaidi na kupunguza
gharama za ujenzi wa majengo.
Mhe.
Dkt. Magufuli ambaye leo ameingia Mkoani Mtwara akitokea Mkoani Lindi
amesimamishwa na wananchi wa Kijiji cha Mnolela Kilichopo Lindi Vijijini
ambapo baada ya kupokea kero ya Kijiji hicho kushindwa kumalizia jengo
la zahanati aliamua kulikagua na kisha akatoa mchango wa Shilingi
Milioni 15, zitakazojumlishwa na Shilingi Milioni 10 zitakazotolewa na
Mbunge wa Jimbo la Mtama Mhe. Nape Nnauye na Shilingi Milioni 30
zitakazotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini, na ameagiza
ujenzi huo ukamilike ndani ya miezi 3 kuanzia sasa.
Halikadhalika,
Mhe. Rais Magufuli amesimamishwa na kuzungumza na wananchi wa Kijiji
cha Madangwa kilichopo Lindi Vijijini ambapo baada ya kupokea kero ya
ubadhirifu wa fedha za wakulima wa Korosho ameuagiza uongozi wa Mkoa wa
Lindi kuwasaka viongozi wote wa vyama vya ushirika wanaotuhumiwa kula
fedha za wakulima na kuwachukulia hatua za kisheria.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Mtwara
04 Machi, 2017
COMMENTS