RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA GATI NAMBA 2 KATIKA BANDARI YA MTWARA PIA AFUNGUA JENGO LA KITUO CHA KIBIASHARA CHA BENKI YA NMB MTWARA

   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akivuta kitambaa pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawas...


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akivuta kitambaa pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi katika Ujenzi wa  Gati namba mbili litakayojengwa katika Bandari ya Mtwara.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Gati namba 2 katika Bandari ya Mtwara.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania  Mhandisi Deusdedit Kakoko kuhusu eneo ambalo Bandari ya Mtwara walikuwa wakilihitaji kutoka sehemu nyingine.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania  Mhandisi Deusdedit Kakoko kuhusu eneo ambalo Bandari ya Mtwara walikuwa wakilihitaji kutoka sehemu nyingine.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka saini katika kitabu cha wageni kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Gati namba 2 litakalojengwa katika bandari ya Mtwara.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mbunge wa Newala George Huruma Mkuchika mara baada ya kuwasili katika eneo la Bandari ya Mtwara.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango Mtkurugenzi Mkuu wa Benki ya NMB Ineke Bussemaker wakikata utepe kuashiaria ufunguzi rasmi wa Kituo cha Biashara cha Benki hiyo mkoani Mtwara
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NMB Ineke Bussemaker, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego wakipiga makofi mara baada ya kufungua kituo hicho cha Kibiashara cha NMB mkoani Mtwara.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NMB Ineke Bussemaker mara baada ya kukifungua kituo hicho cha kibiashara mkoani Mtwara.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mbunge wa Mtwara mjini kupitia Chama cha Wananchi (CUF) Maftah Nachuma mara baada ya kufungua kituo hicho cha kibiashara cha Benki ya NMB mkoani Mtwara.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Mbunge wa Mtama Nape Nnauye kuhusu ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mnolela ambapo pia amechangia kiasi cha Shilingi milioni 15 na akamuagiza Mbunge huyo kuchangia Shilingi milioni 10 kutoka fedha za jimbo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika kijiji cha Madangwa katika jimbo la Mtama mkoani Lindi.
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM na Mbunge mteule wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete akifUatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati aliposimamishwa njiani na Wanakijiji wa Madangwa katika jimbo la Mtama mkoani Lindi. (PICHA NA IKULU)
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULUDescription: Description: Description: Description: Description: Coat of Arms
Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz               

Faksi: 255-22-2113425



OFISI YA RAIS,
     IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,   
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kuachana na utaratibu wa kutoa zabuni za uendeshaji wa bandari kwa kampuni binafsi ambazo huingia mikataba isiyo na manufaa kwa nchi na kusababisha uwepo mianya ya upotevu wa fedha za umma.
Mhe. Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 04 Machi, 2017 muda mfupi kabla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa gati namba 2 ya bandari ya Mtwara ambayo ujenzi wake unatarajiwa kuchukua muda wa miezi 21 kuanzia sasa.
"Kwa sababu mmeamua kuichimba hii bandari ili kuongeza kina mpaka mita 15 kwa kutumia fedha zetu, sitegemei TPA na Wizara kuingia tena mkataba na wawekezaji wengine, kwa sababu imekuwa ni kawaida hapa Tanzania, tunatumia fedha zetu halafu wanakuja watu wengine kufanya biashara na fedha zetu kana kwamba nchi hii haina wasomi, na wanaokuja kuendesha kweli wanaiba" amesema Mhe. Rais Magufuli.
Mapema Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema gati namba 2 itakayojengwa katika bandari ya Mtwara itakuwa na urefu wa mita 350 na ujenzi wake utagharimu Shilingi Bilioni 137.5 zote zikiwa zimetolewa na Serikali ya Tanzania.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mhandisi Deusdedit Kakoko amesema imelazimu kuongeza gati katika bandari ya Mtwara baada ya kuwepo ongezeko la mizigo inayosafirishwa kupitia bandari hiyo ambapo kiwango cha mizigo inayohudumiwa kinatarajiwa kuongezeka kutoka tani 273,886 mwaka 2015/2016 hadi kufikia tani 388,000 mwaka 2016/2017 kiwango ambacho kinakaribia ukomo wa uwezo wa bandari hiyo yenye uwezo wa kuhudumia tani 400,000 kwa mwaka.
Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amefungua Kituo cha Biashara cha Benki ya NMB Mjini Mtwara na kutoa maagizo kwa Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango kutoa maelekezo ili fedha zote za Serikali zipitie Benki ya NMB ambayo licha ya hisa zake kumilikiwa na Serikali kwa asilimia 32 imekuwa ikitoa gawio kwa Serikali kila mwaka ambapo mwaka 2016 ilitoa Shilingi Bilioni 16.5 na mwaka huu inatarajia kutoa zaidi ya kiwango hicho cha gawio.
"Na nikuombe Waziri, kwa sababu wewe ndio unayesimamia fedha za Serikali, toa maelekezo ili fedha zote zipitie benki ya NMB, labda kama kutakuwa na umuhimu sana wa kupitia benki nyingine" amesema Mhe. Rais Magufuli.
Mhe. Rais Magufuli ambaye ameipongeza benki ya NMB kwa kujikita kutoa huduma za kibenki kwa wananchi wa kawaida na wafanyakazi nchi nzima ametoa wito kwa benki zote nchi kupunguza viwango vya riba ili Watanzania wengi waweze kukopa na kufanya shughuli za uzalishaji mali.
Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Magufuli amefungua jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Mjini Mtwara ambalo limejengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 31 na linatoa huduma za Benki Kuu katika kanda ya kusini inayojumuisha Mikoa ya Mtwara, Lindi na sehemu za Mikoa ya Pwani na Ruvuma.
Pamoja na kumpongeza Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuridhia ujenzi wa jengo hilo na kuipongeza BOT kwa kufanikisha ujenzi huo na kusimamia vizuri uchumi wa nchi, Mhe. Rais Magufuli ameitaka benki hiyo kuu kuchukua hatua kali dhidi ya benki ambazo zimekuwa zikikiuka maadili na taratibu za kibenki ikiwemo kushiriki njama za kuiba fedha za Serikali kupitia mikopo na utakatishaji wa fedha.
Aidha, amemtaka Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Benno Ndulu aandae utaratibu utakaozibana benki zinazofanya biashara hapa nchini ili zilazimike kuwakopesha wananchi, kupunguza viwango vya riba na kuendeleza shughuli za uzalishaji mali.
Mhe. Rais Magufuli pia amefungua nyumba 40 za makazi za Rahaleo zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mjini Mtwara kwa gharama ya Shilingi Bilioni 10.5 na ameipongeza NHC kwa kazi nzuri ya ujenzi wa nyumba za makazi ya wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.
Akiwa katika mradi huu Mhe. Dkt. Magufuli ameagiza kuanzia sasa Mkoa, Wilaya ama Kiongozi yeyote atakayeomba kujengewa makazi na NHC ahakikishe eneo lililoandaliwa kwa ajili ya kujengwa makazi hayo linafikishiwa barabara, umeme na maji na ameitaka NHC kuacha kutumia wakandarasi katika ujenzi wa majengo yake na badala yake waunde vikosi kazi vya ujenzi kwa kutumia wataalamu waliopo ndani ya nchi ili kuzalisha ajira zaidi na kupunguza gharama za ujenzi wa majengo.
Mhe. Dkt. Magufuli ambaye leo ameingia Mkoani Mtwara akitokea Mkoani Lindi amesimamishwa na wananchi wa Kijiji cha Mnolela Kilichopo Lindi Vijijini ambapo baada ya kupokea kero ya Kijiji hicho kushindwa kumalizia jengo la zahanati aliamua kulikagua na kisha akatoa mchango wa Shilingi Milioni 15, zitakazojumlishwa na Shilingi Milioni 10 zitakazotolewa na Mbunge wa Jimbo la Mtama Mhe. Nape Nnauye na Shilingi Milioni 30 zitakazotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini, na ameagiza ujenzi huo ukamilike ndani ya miezi 3 kuanzia sasa.
Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli amesimamishwa na kuzungumza na wananchi wa Kijiji cha Madangwa kilichopo Lindi Vijijini ambapo baada ya kupokea kero ya ubadhirifu wa fedha za wakulima wa Korosho ameuagiza uongozi wa Mkoa wa Lindi kuwasaka viongozi wote wa vyama vya ushirika wanaotuhumiwa kula fedha za wakulima na kuwachukulia hatua za kisheria.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Mtwara
04 Machi, 2017

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA GATI NAMBA 2 KATIKA BANDARI YA MTWARA PIA AFUNGUA JENGO LA KITUO CHA KIBIASHARA CHA BENKI YA NMB MTWARA
RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA GATI NAMBA 2 KATIKA BANDARI YA MTWARA PIA AFUNGUA JENGO LA KITUO CHA KIBIASHARA CHA BENKI YA NMB MTWARA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh9jve_ePFQQy2h3z074rtig4ijlU5hMOko3JK7kpS3PWovPuSw26kRMQIYzMLej_fCenyDP1BEhgeIeZV1SA5vW78qpeHuen7y88t29qpmO6m0e38NnX08uFp1CzpIxs6AW-KOsyae0dBs/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh9jve_ePFQQy2h3z074rtig4ijlU5hMOko3JK7kpS3PWovPuSw26kRMQIYzMLej_fCenyDP1BEhgeIeZV1SA5vW78qpeHuen7y88t29qpmO6m0e38NnX08uFp1CzpIxs6AW-KOsyae0dBs/s72-c/1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/rais-dkt-magufuli-aweka-jiwe-la-msingi.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/rais-dkt-magufuli-aweka-jiwe-la-msingi.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy