Na. Immaculate Makilika- MAELEZO Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ...
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi
katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yanayotarajiwa kufanyika
Machi 8 Mwaka huu, katika uwanja wa Mwembeyanga Temeke Jijini Dar es
Salaam.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
jana maadhimisho hayo yataongozwa na maandamano ya Wanawake na wadau
mbalimbali, na yataanzia katika Shule ya Msingi Mabatini kuelekea
viwanja vya Mwembeyanga.
Maadhimisho
ya Siku ya Wanawake Duniani Mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu isemayo
“Tanzania ya viwanda, Wanawake ndio Msingi wa Mabadiliko ya Kiuchumi”.
Kauli
mbiu hiyo inalenga kuikumbusha jamii kuhusu umuhimu wa kujenga mazingira
wezeshi kwa Wanawake hasa kutambua mchango wao katika kuleta Maendeleo
yao na ya jamii kwa ujumla.
Taarifa
hiyo pia imeikumbusha jamii kuhusu wajibu wake ikiwa ni pamoja na
kuwashirikisha, kuwaamini na kuwapa Wanawake haki sawa katika nafasi za
Elimu, Uchumi na uongozi ili wawe chachu ya mabadiliko yenye lengo la
kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
Maadhimisho
hayo yataambatana na maonesho ya kazi za ujasiriamali yanayoendelea
katika uwanja wa Mwembeyanga, ambapo Asasi za kiraia na vikundi
mbalimbali vya wanawake vitaonesha bidhaa zao.
Aidha,
Wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam wanakumbushwa kushiriki kwa wingi
katika maadhimisho hayo ikiwa ni pamoja na kuwa na mikakati ya
kukabiliana na changamoto mbalimbali zinanazowakabili Wanawake kuanzia
ngazi ya kaya hadi Taifa.
COMMENTS