MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA ALAANI NA KUKEMEA VIKALI VITENDO VYA UKEKETAJI WA WANAWAKE NA UBAKAJI VINAVYOENDELEA KATIKA JAMII

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amelaani na kukemea vikali vitendo vya ukeketaji wa wan...


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amelaani na kukemea vikali vitendo vya ukeketaji wa wanawake na ubakaji vinavyoendelea katika jamii na amewataka wananchi kote nchini kushirikiana katika kukabiliana na vitendo hivyo nchini.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo tarehe 8-March-2017 wakati akizungumza katika mahojiano maalum na Shirika la Utangazaji wa Tanzania (TBC) mjini Dodoma kuhusu maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema vitendo hivyo vya ukeketaji wa wanawake na ubakaji vinamchukiza sana hivyo ametoa wito maalum kwa wananchi na wadau wote bila kujadili dini, kabila wala rangi kupambana ipasavyo na vitendo hivyo ambavyo vinarudisha nyuma jitihada za kumkwamua mwanamke kiuchumi.

Kuhusu maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema anafurahishwa na hatua na jitihada zinazochukuliwa na wanawake kote nchini katika kujikwamua kiuchumi kwa kuimarisha shughuli zao za ujasiriamali katika kuelekea katika uchumi wa viwanda.

Amesema jukumu kubwa la serikali ya awamu ya Tano ni kuhakikisha wanawake wanaboreshewa ipasavyo mazingira ya kufanyia kazi hasa shughuli za ujasiriamali ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea.

“Inapofika katika shida zetu wanawake ni lazima tuwe na kitu Kimoja na sauti Moja katika kulinda na kutetea haki zetu bila kujali itikadi za kisiasa”Amesisitiza Makamu wa Rais.

Katika uundaji wa majukwaa ya kuwawezesha wanawake kiuchumi nchini, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kazi hiyo inaendelea vizuri na kutaka mikoa na wilaya ambazo bado haijaunda majukwaa hayo kufanya hivyo haraka iwezekanavyo.

Ameeleza kuwa lengo la uundaji wa majukwaa hayo katika ngazi ya wilaya na mikoa nchini ni kuwakutanisha wanawake pamoja katika kujadili na kutafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili ikiwemo tatizo la masoko za bidhaa wanazozizalisha.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa majukwaa hayo ambayo yameanza kuundwa katika mikoa mbalimbali nchini yatakuwa sio ya kisiasa.

Katika Mahojiano hayo na mtangazaji Shaban Kissu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) mjini DODOMA, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu ametumia sehemu ya mahojiano hayo kwa kuwatakia heri na mafanikio wanawake wote nchini katika kuadhimisha Siku ya wanawake Duniani.

Kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya wanawake Duniani ni “Tanzania ya Viwanda,Wanawake ni msingi wa mabadiliko ya Kiuchumi”.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
Dodoma. 8-Mar-2017

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA ALAANI NA KUKEMEA VIKALI VITENDO VYA UKEKETAJI WA WANAWAKE NA UBAKAJI VINAVYOENDELEA KATIKA JAMII
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA ALAANI NA KUKEMEA VIKALI VITENDO VYA UKEKETAJI WA WANAWAKE NA UBAKAJI VINAVYOENDELEA KATIKA JAMII
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvuRUba3b3H9qnnIlSLxS6mrcZwGNJ3N_YUfkw994aS1dvLI5f1v57vDtxZrmf82qi3eHo2cT09u7RC61ilEmIY8G7MjyfAxX8I72aV2zviGJ-8DhiaRPcZvoauEKZ0E71IuCc2kcA0eA/s400/unnamedy.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvuRUba3b3H9qnnIlSLxS6mrcZwGNJ3N_YUfkw994aS1dvLI5f1v57vDtxZrmf82qi3eHo2cT09u7RC61ilEmIY8G7MjyfAxX8I72aV2zviGJ-8DhiaRPcZvoauEKZ0E71IuCc2kcA0eA/s72-c/unnamedy.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/makamu-wa-rais-mhe-samia-alaani-na.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/makamu-wa-rais-mhe-samia-alaani-na.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy