JOKATE AANZISHA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KWA WANAFUNZI WA KIKE

Mrembo mwenye vipaji lukuki nchini, Jokate Mwegelo ameanzisha mpango maalum wa kufundisha somo la ujasiriamali kwa wanafunzi wa kid...


Mrembo mwenye vipaji lukuki nchini, Jokate Mwegelo ameanzisha mpango maalum wa kufundisha somo la ujasiriamali kwa wanafunzi wa kidato cha pili wa shule ya sekondari ya Majani ya Chai iliyopo Vingunguti katika Manispaa ya Ilala.

Jokate ataanza mafunzo hayo maalum kwa wanafunzi wa kike kuanzia wiki ijayo na lengo la mafunzo hayo ni kuwapa ufahamu wanafunzi hao na kuanzisha biashara zao mara baada ya kumaliza elimu yao ya sekondari.

Alisema kuwa mafunzo ya ujasiriamali kwa wanafunzi ni muhimu kwani yanawawezesha kujiandaa vizuri kukabiliana na maisha mara baada ya kuhitimu masomo yao ya sekondari na kushindwa kuendelea na masomo ya ngazi ya juu.Kwa mujibu wa Jokate, unaweza kusoma mpaka Chuo Kikuu ndani na nje ya nchi, lakini bado utakabiliana na ugumu wa kupata ajira ambazo kwa sasa ni haba.

“Kuna wengine wamesomea taaluma fulani  kwa ngazi ya Chuo Kikuu lakini mpaka sasa hawana ajira na kukata tama katika maisha, pia unaweza kufanya kazi tofauti na taaluma uliyosomea, lakini kwa ujasiriamali ni tofauti, utajifunzi jinsi ya kupata mtaji, kukopa na kurejesha, kufanya biashara gani na mbinu zake,”

“Mfano halisi mimi mwenyewe, nimesomea mambo tofauti na kazi ninazozifanya ni tofauti, ni mbunifu wa mitindo, mavazi, muigizaji wa filamu, mwanamuziki na pia ni mfanyabiashara, haya yote sikusomea, ila najivunia kwani ndiyo yanaendesha maisha yangu, wanafunzi wana vipawa tofauti, naamini katika programu hii nitapata wengi na kupata mafanikio,” alisema Jokate.

Alisema kuwa atakuwa anafundisha mafunzo hayo mara moja kwa wiki kuanzia wiki ijayo. “Nimeamua kuanza rasmi siku ya wanawake duniani, maandalizi yamekamilika na nawaomba wanafunzi wajiandae kwani mafunzo ni mazuri na yatawajengea moyo wa kujiamini kwani si kila anayesoma anatakiwa kuajiliwa,” alisema.
Jokate Mwegelo akicheza muziki na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Majani ya Chai ya Ilala wakati wa mahafari ya mwaka jana.
Jokate Mwegelo akikabidhi zawadi kwa mmoja wa mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Majani ya Chai wakati wa maafali ya mwaka jana ya kidato cha nne.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: JOKATE AANZISHA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KWA WANAFUNZI WA KIKE
JOKATE AANZISHA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KWA WANAFUNZI WA KIKE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhS0IbWGUmcFNegS-12cGtjSirpgVT51otBYKzl2KkVsi71lxRfsz3nHLXmNkmr9TXZ67Ww53Zix0RR2FS0tVDJkBWlqHWElA5EghDOzqDMDWQF8e0WeBMWn52XmviB0d_iCpWNO8ftx-c/s640/JOKATE+1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhS0IbWGUmcFNegS-12cGtjSirpgVT51otBYKzl2KkVsi71lxRfsz3nHLXmNkmr9TXZ67Ww53Zix0RR2FS0tVDJkBWlqHWElA5EghDOzqDMDWQF8e0WeBMWn52XmviB0d_iCpWNO8ftx-c/s72-c/JOKATE+1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/jokate-aanzisha-mafunzo-ya-ujasiriamali.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/03/jokate-aanzisha-mafunzo-ya-ujasiriamali.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy