MBUNGE LEMA AZUA TAHARUKI UZINDUZI WA UJENZI WA HOSPITALI ARUSHA LEO.

VURUGU kubwa zimeibuka baina ya Mkuu wa Mkoa Arusha Mrisho Gambo na mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema katika hafla y...









VURUGU kubwa zimeibuka baina ya Mkuu wa Mkoa Arusha Mrisho Gambo na mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika hospitali ya mama na mtoto inayojengwa eneo ya Buruka nje kidogo ya jiji la Arusha.

Vurugu hiyo zimeibuka baada ya mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kuvuruga ratiba iliyokuwa imepagwa na waandaaji wa hafla hiyo ambapo kwa mujibu wa ratiba hiyo ilikuwa imepagwa kuwa hotuba ya mkuu wa mkoa ingetanguliwa na waandaji wa shughuli hiyo akiwemo waandaji wa hafla hiyo, wafadhili pamoja na Mbunge Lema.

Kabla ya vurugu hizo mkuu wa Mkoa wa Arusha alikaribishwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru, Alexzanda Mnyeti swala ambalo liliibua mzozo mkubwa kwa wananchi walikuwa wamefika kushuudia tukio hilo la uzinduzi wakiwemo wafadhili waliofadhili mradi ambao ni shirika la kuhudumia afya ya mama na mtoto (Maternity Afrika ).

Baada ya kuanza kuhutubia mkuu huyo wa mkoa akielezea historia ya mradi huo ikiwepo upatikanaji wa eneo la kujenga mradi wa hospitali hiyo ghafla mbunge Lema alisimama na kupinga hotuba hiyo na kudai imejaa upotoshwaji na siasa ndani kwani yeye ndiye aliyetafuta eneo hilo la ujenzi wa hospitali hiyo kutoka kampuni ya mawala Advocate na siyo kweli eneo hilo limetokana na maono aliyokuwa nayo Marehemu Advocate Nyaga Mawala ya muda mrefu .
 
 
Picha ikionyesha wa (kushoto) mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiwa anatulizwa na mchungaji, Wilfred Mlayi, wakati mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo (kulia)  akiwa anatulizwa na mfadhili wa Mradi huo ambaye ni daktari bigwa wa magonjwa ya kina mama na Mtoto Duniani Edru Broun.
 
Wananchi waliohudhuria uzinduzi wa ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto ambaye akupenda kutaja jina lake akiwa anamuomba mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema kutulia na kumuaacha mkuu wa mkoa aendelee kutoa hutuba. (Habari picha na Woinde Shizza, Arusha).
 
Kwa upande wake mwenyekit wa Tasisi ya maendeleo ya jiji la Arusha (ARDF) Elifuraha Mtowe Alisema kuwa eneo la kujegwa hospitali hiyo lilitolewa na marehemu Nyaga Mawala nakwa ARDF kupitia ofisi ya mbunge wa jimbo la Arusha mjini ndipo taasisi yao ya ARDF ikamamua kutafuta mfadhili ndipo walipompata Martenity Afrika.

Alisema kuwa tangu wampate mfadhili waliingia mkataba na wakakubaliana hospitali iishe ndani ya mika mitano lakaini mfadhili mwenyewe aliwaakikishia kuwa hospitali hiyo itaisha mapema iwezeka kwani itakamilika ndani ya mwaka mmoja tu ili mama na mtoto aweze kupata huduma kwa araka zaidi.

Awali mbunge Lema aliwaambia waandishi wa habari kuwa mkuu wa mkoa huyo alikuwa amegoma kuja kuzindua hospitali hiyo hadi pale mbunge huyo alipoamua kumpiga simu katibu mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi na kumwambia kuwa mkuu wa mkoa kagoma kuja kuzindua hospitali hiyo ndipo katibu mkuu alipoamua kupiga simu wizara ya TAMISEMI ambapo ndio walimpigia simu mkuu wa mkoa ili aweze kufika kwenye uzinduzi huo.
 



COMMENTS

BLOGGER: 2
Loading...
Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MBUNGE LEMA AZUA TAHARUKI UZINDUZI WA UJENZI WA HOSPITALI ARUSHA LEO.
MBUNGE LEMA AZUA TAHARUKI UZINDUZI WA UJENZI WA HOSPITALI ARUSHA LEO.
https://i.ytimg.com/vi/kJvtrhkeBRo/hqdefault.jpg
https://i.ytimg.com/vi/kJvtrhkeBRo/default.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/mbunge-lema-azua-taharuki-uzinduzi-wa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/10/mbunge-lema-azua-taharuki-uzinduzi-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy