OMUTWALE Paschal Rutaihwa Kakiziba 13 JULAI 1935 – 28 OKTOBA 2004 Baba yetu mpendwa umetimiza mwaka wa 12 tangu...
OMUTWALE Paschal Rutaihwa Kakiziba
13 JULAI 1935 – 28 OKTOBA 2004
Baba
yetu mpendwa umetimiza mwaka wa 12 tangu ulipotwaliwa na Bwana. Picha
yako inatukumbusha uwepo wako tulipokuwa sote hapa duniani, na hasa
ukarimu, upendo, upole, uchangamfu na wingi wa busara.
Ni
vigumu kukubali kwamba haupo nasi lakini hatuna budi kuamini kwamba uko
nasi kiroho kwa vile tunaye Mungu ambaye anaendelea kututia nguvu kila
iitwapo leo. Busara zako na ucheshi wako vinazidi kutuimarisha kila siku
na tunaendelea kuzingatia maneno yako uliyokuwa ukihimiza juu ya kuwa
na upendo na umoja katika familia huku tukiendelea kumtumaini Mungu wetu
ambaye amekuita kwake.
Mke
wako Mary-Hilda Kakiziba, rafiki yako Galita, watoto wako, wajukuu,
wakwe zako, dada zako, kaka zako na wadogo zako, ndugu, marafiki na
majirani wanakosa ucheshi na ushauri wako na wanakukumbuka daima. MISA
YA KUMBUKUMBU ITAFANYIKA JUMAPILI, OKTOBA 30, 2016, SAA 3 ASUBUHI KWENYE
KIGANGO CHA MT. ANTHONY WA PADUA, BOKO, DSM.
Tumaini
letu linajengwa na neno lisemalo: ”Umevipiga vita vilivyo vizuri,
mwendo umeumaliza na imani umeilinda” (2Tim. 4:7) Tunakuomba Ee Bwana
uendelee kuipumzisha roho yake mahali pema peponi, AMEN.
COMMENTS