Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Deogratius Ndejembi akizungumza wakati wa kikao cha Kumng'oa Meneja wa Mamlaka ya Maji saf...
Mkuu
wa Wilaya ya Kongwa Mhe Deogratius Ndejembi akizungumza wakati wa kikao
cha Kumng'oa Meneja wa Mamlaka ya Maji safi na salama Wilyani humo.
Watumishi wa Mamlaka ya Maji safi na salama WIlayani Kongwa wakizunguza na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Deogratius Ndejembi
Na Mathias Canal, Dodoma
Kushindwa kusimamia miundombinu ya maji na kupelekea kuwa na ugumu wa
upatikanaji maji kwa kiwango kinachotakiwa ni miongoni mwa kadhia
zilizopingwa wakati wa kampeni na Mgombea Urais kupitia tiketi ya Chama
Cha Mapinduzi (CCM) Ambaye ndiye Rais wa Tanzania Dkt John Pombe
Magufuli na kuahidi kuchagua wasaidizi watakaosimamia na kulimaliza
jambo hilo mara baada ya kuingia madarakani.
Kwa kiasi kikubwa
nchini Tanzania kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi wakitupa
lawama kwa baadhi ya watendaji wa serikali ambao wamesababisha kudorora
kwa uchumi na kuchagiza ugumu wa maisha kutokana na umbali wanaotumia
kutafuta maji, huduma za afya sambamba na umbali wa shule za Sekondari
na Msingi.
Kutokana na kadhia ya upatikanaji hafifu wa maji safi
na salama Wilayani Kongwa imepelekea kukalia kuti kavu kwa Meneja wa
Mamlaka ya Maji safi na Salama Wilayani humo Ndg Kisha Bonga kutokana na
kushindwa kusimamia majukumu yake ipasavyo ikiwemo kusababisha
wafanyakazi wa Mamlaka ya maji kufikia maamuzi ya kuandamana. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
COMMENTS