Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni kabla ya kuanza kwa Mkutano wa African Pee...
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Uganda,
Yoweri Museveni kabla ya kuanza kwa Mkutano wa African Peer Review
Mechanism Forum (APRM)kwenye ukumbi wa hoteli ya Intercontinental jijini
Nairobi Agosti 26, 2016. (PICHA NA OFISI
YA WAZIRI MKUU)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na ujumbe wake wakishiriki katika Mkutano
wa African Peer Review Mechanism Forum (APRM)kwenye ukumbi wa hoteli ya
Intercontinental jijini Nairobi Agosti 26, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika
maungumzo na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya (kulia), Rais wa Msumbiji,
Filipe Nyusi (wapili kulia) na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU),
Madame Nkosazana Dlamini- Zuma kabla ya kuanza kwa Mkutano wa African Peer
Review Mechanism Forum (APRM) kwenye ukumbi wa hoteli ya Intercontinental
jijini Nairobi Agosti 26, 2016
MAJALIWA AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS WA JICA JIJINI NAIROBI
Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa akizungumza na Makamu
wa Rais wa Shirika la Kimataifa la Misaada la Japan (JICA) Bw. Hiruchi
Kato (kulia kwake) na ujumbe wake, jijini Nairobi Agosti 26, 2016 ambako
anatarajiwa kuhudhuria mkutano wa sita Wa Tokyo International Conference
o n Africa Development (TCAD). Kushoto kwake ni Balozi wa Tanzania nchini Japan
Mathias Chikawe. (PICHA NA OFISI YA
WAZIRI MKUU)
*Kampuni Chiyoda kufundisha
Watanzania masuala ya gesi
*JICA kusaidia ujenzi wa
miundombinu Dodoma
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa
amewasili Nairobi, Kenya kuhudhuria Mkutano wa Mkuu wa Sita wa Wakuu wa Nchi wa
TICAD (TICAD VI) utakaofanyika Agosti 27 -28, mwaka huu. Waziri Mkuu
anahudhudia mkutano huo kwa niaba ya Rais, Dk. John Pombe Magufuli.
Leo asubuhi (Ijumaa, Agosti
26, 2016) Waziri Mkuu amekutana na viongozi wakuu mbalimbali wa makampuni ya
kibiashara kutoka Japan ambao wamekuja kuhudhuria mkutano huo.
Waziri Mkuu amekutana na
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Chiyoda Corporation, Bw. Tadashi Izawa ambapo
katika mazungumzo yao, pamoja na kuangalia fursa nyingine katika sekta ya gesi
Tanzania, kampuni hiyo imekubali kutoa mafunzo ya kujenga uwezo wa wataalamu
kwa sekta ya gesi hususan usindikaji wa gesi kwa ajili ya kusafirisha nje ya
nchi (Liquefied Natural Gas).
Bw. Izawa amemweleza Waziri
Mkuu kwamba wamefurahiswa na taarifa za ugunduzi wa gesi ya Helium hapa nchini
Tanzania na kwamba kampuni yake ina teknolojia na uzoefu wa muda mrefu katika
kutekeleza miradi ya gesi (Gas value Chain Planning and Execution).
“Tunao uzoefu wa muda mrefu,
pia tunazo teknolojia za kuendeleza sekta ya gesi ikiwemo Helium kwa mfano
ujuzi wa kutenganisha gesi asilia na helium (Separation of Natural Gas and
Helium). Tumetekeleza miradi ya namna hii nchini Qatar ambayo kwa sasa ni ya
pili kwa uzalishaji wa gesi hiyo duniani ikitanguliwa na Marekani,” amesema.
Amesema mafunzo hayo
yatafanyika kuanzia mwakani na yatalenga vijana wasiopungua 10 kutoka Tanzania
ambao wamehitimu shahada za uhandisi kwani wameshafanya hivyo kwa vijana wanane
kutoka Msumbiji.
Waziri Mkuu alimshukuru Vw.
Izawa kwa mpango wao wa mafunzo kwa vijana wa Kitanzania lakini akamtaka pia
waangalie uwezekano wa kuwasaidia vijana wanaotoka maeneo husika yenye gesi ili
wapatiwe mafunzo ambayo yatawawezesha kumudu baadhi ya kazi kwenye viwanda vya
kusindika gesi.
Wakati huohuo, Waziri Mkuu amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa
Rais wa Shirika la Misaada ya Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Hiroshi Kato na
kujadiliana mambo kadhaa yakiwemo ya nishati na miundombinu.
Katika mazungumzo hayo, Bw.
Kato alimweleza Waziri Mkuu nia ya shirika hilo kuendelea kusaidia miradi
mbalimbali ya kilimo hapa nchini na hasa katika sekta za afya, maji, kilimo na
miundombinu ambazo imekuwa ikijihusisha nazo kwa muda mrefu sasa.
Waziri Mkuu alimshukuru kwa
ushiriki wa shirika hilo kwenye miradi ya nishati ya Kinyerezi na akamtaka
aendelee kuisaidia Serikali ya Tanzania inainginia kwenye awamu ya tatu ya
Kinyerezi (Kinyerezi III).
Katika hatua nyingine, Balozi
wa Tanzania nchini Japan, Mathias Chikawe alimwoba makamu wa Rais hyo waangalie
uwezekano wa kuwekeza kwenye sekta za nishati na miundombinu ya mkoa Dodoma
hasa katika kipindi ambacho Serkali imeamua kuhamia huko.
“Tunaomba muangalie sana
suala la kuendeleza nishati ya umeme kwani nchi yetu imeamua kuwa nchi ya viwanda.
Tutahitaji kuwa na umeme wa kutosha kuendesha viwanda vya usindikaji bidhaa
zetu, lakini pia si mbaya mkiangalia suala la kuboresha miundombinu ya barabara
na usafirishaji katika mji wa Dodoma,” amesema.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, AGOSTI 26, 2016.
COMMENTS