PSPF YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA JESHI LA MAGEREZA UKONGA JIJINI DAR ES SALAAM

Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (kushoto), akimkabidhi seemu ya vifaa vya michezo, Mkuu wa K...








Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (kushoto), akimkabidhi seemu ya vifaa vya michezo, Mkuu wa Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari, Agosti 25, 2016. Vifaa hovyo ni vya michezo ya ngumi, mpira wa miguu na mpira wa pete.
 Afisa Masoko wa PSPF, Magira Werema, (kushoto), akimkabidhi sehemu ya vifaa hivyo, Mkuu wa Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Ukonga jijini
Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari.


NA
K-VIS BLOG/KHALFAN SAID



MFUKO
wa Pensheni wa PSPF, umekabidhi vifaa vya michezo kwa wanamichezo wa Jeshi la
Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam na kasha kufuatiwa na PSPF bonanza la michezo ya mpira wa miguu, mpira wa pete, Ngumi na
Judo.
Akikabidhi
vifaa hivyo vya michezo Agosti 25, 2016, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko
huo, Abdul Njaidi, alisema, PSPF imeamua kutoa vifaa hivyo ili kuunga mkono juhudi
za serikali katika kuinua michezo nchini.
“Nyinyi
mkiwa kama sehemu kubwa ya wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, tunayo
furaha kutoa vifaa hivi vya michezo kwani baada ya kutekeleza majukumu mazito
ya kitaifa mnahitaji kushiriki michezo ili kujenga afya lakini pia kuinua
vipaji vyenu,” alisema na kuongeza,
 “Nichukue fursa hii kuwahamasisha mjiunge na
PSPF kwani kuna faida nyingi mtapata kutokana na kutoa mafao mbalimbali yatakayoboresha
maisha yenu kama ambavyo kauli mbiu yetu inavyosema, PSPF ni chaguo lako sahihi
na kamwe hutajutia uamuzi wako wa kujiunga na Mfuko huu.” Alisisitiza Njaidi.
Akipokea
vifaa hivyo kwa niaba ya wanamichezo hao, Mkuu wa Kikosi Maalum cha
Magereza-Ukonga, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari,
aliishukuru PSPF kwa msaada huo wa vifaa vya michezo kwani vitawawezesha
wanamichezo hao kushiriki michezo katika mazingira bora ya kiuanamichezo.
Baada
ya makabidhiano hayo, wanamichezo hao walionyesha uwezo wao katika michezo ya
mpira wa miguu, ngumi, mpira wa pete, na judo.

 Afisa Matekelezo (Compliance), wa PSPF, George Mnasizu, (kushoto), akigawa vipeperushi vyenye maelezo ya kina ya huduma zitolewazo na Mfuko huo kwa baadhi ya wanamichezo wa Jeshi la Magereza
 Njaidi akiwa na Mkuu wa Kikosi hicho, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kikosi Maalum cha Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, Rajabu Nyange Bakari, na wacheza judo wa kikosi hicho wakiwa katika picha ya pamoja na vipeperushi vya PSPF.
 Njaidi akimkabidhi sehemu ya vifaa hicho, Nahodha wa timu ya mpira wa pete (Netball), wa timu ya Magereza Ukonga, Pili Enzi
 Werema akimkabidhi sehemu ya vifaa hivyo kocha wa soka wa timu ya Magereza, Sajenti Hassan Mulego
 Njaidi akikagua timu ya soka ya Magereza Ukonga, ambayo ilimenyana na Kikosi Maalum cha Magereza Dar es Salaam, wakati wa bonanza hilo la michezo
  Soka likiendelea baina ya Kikosi Maalum na timu ya Magereza

  Soka likiendelea baina ya Kikosi Maalum na timu ya Magereza

  Soka likiendelea baina ya Kikosi Maalum na timu ya Magereza

 Hizi ndio Gloves na flana zilizotolewa kwa wana masumbwi (ngumi)
 Pambano la masumbwi likiendelea
  Pambano la masumbwi likiendelea
 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi, akiwa na Mkuu wa Kikosi Maalum cha Magereza jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari, wakati akitoa nasaha kwa wanamichezo kabla ya kuanza kwa bonanza hilo
Nasaha za mgeni rasmi kwa wanamichezo
 Wanamichezo wakishangilia hotuba
 Onyesho la Judo
 Werema akimkabidhi sehemu ya vifaa hivyo vya michezo, Kocha na Afisa Michezo wa Kikosi Maalum cha Magereza Dar es Salaam, Inspekta Francis Tabu
 Soka likiendelea baina ya Kikosi Maalum na timu ya Magereza




COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: PSPF YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA JESHI LA MAGEREZA UKONGA JIJINI DAR ES SALAAM
PSPF YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA JESHI LA MAGEREZA UKONGA JIJINI DAR ES SALAAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgci1Y49Q-T0e4xyrhUKD7TG_XWVAKE16PrW9mZsdjTK-zCxP5LSS_BD1GQeHthq-49fLdbVYv8d2j_9aiAtxyHGFVKmwYcG1kSUKzavYpQyaKZ0WoTlcUmKJIHkSVnXj0qNDvrbrAv27E/s640/Daily+News.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgci1Y49Q-T0e4xyrhUKD7TG_XWVAKE16PrW9mZsdjTK-zCxP5LSS_BD1GQeHthq-49fLdbVYv8d2j_9aiAtxyHGFVKmwYcG1kSUKzavYpQyaKZ0WoTlcUmKJIHkSVnXj0qNDvrbrAv27E/s72-c/Daily+News.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2016/08/pspf-yakabidhi-vifaa-vya-michezo-kwa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/08/pspf-yakabidhi-vifaa-vya-michezo-kwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy