ALIYEKUWA mgombea urais wa Tanzania kupitia CHADEMA mwaka 2015 akiungwa mkono na vyama vinavyounda vuguvugu la U...
ALIYEKUWA
mgombea urais wa Tanzania kupitia CHADEMA
mwaka 2015 akiungwa mkono na vyama vinavyounda vuguvugu la Umoja wa
Katiba ya Wancnhi (UKAWA), Edward Lowassa, na viongiozi wa juu wa chama
hicho wamekamatwa jijini Dar es Salaam alasiri hii Agosti 29, 2016.
Kwa
mujibu wa Mwanasheria Mkuu wa
CHADEMA, Tundu Lissu, wengine waliotiwa mbaroni na polisini pamoja na
Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dkt. Vincent
Mashinji, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, (Zanzibar) na Mbunge wa Goba,
John Mnyika.
Kwa
mujibu wa Lissu, viongzi hao wamekamatwa wakati wakishiriki kikao cha
Kamati Kuu ya chama hicho kilichokuwa kikifanyika hoteli ya Giraffe
Mbezi Beach nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Polisi ilipiga marufuku mikutano yote ya siasa iwe nje au ndani ya ukumbi.
Hata hivyo marufuku hayo ya polisi yamekuwa yakipingwa vikalina wanasiasa hao huku wakishikilia kuwa ni haki yao ya Kikatiba.
CHADEMA
imeingia kwenye msuguano na polisi kufuatia kutangaza operesheni UKUTA
kuanzia Septemba Mosi mwaka huu itakayofanyikanchi nzima hali ambayo kwa
takriban wiki kadhaa sasa, imezua mivutano na baina ya polisi na
chamahicho kikuu cha upinzani huku rai mbalimbali kutoka kila kona,
zikihimiza kufanya maridhiano ili kutuliza "joto" hilo. adi kufikia saa
12;30 jioni hii, viongozi hao walikuwa wakishikiliwa kituo kikuu cha
polisi kati jijini Dar es Salaam, na hakuna Mwandishi wa habari
aliyeruhusiwa kuingia kwenye kituo hicho na kuamriwa kukaa mbali na
kituo.
Hali kadhalikawafuasi na wabunge wa chama hicho wamejikusanya jirani na kituo hicho cha polisi wakisubiri hatma ya viongozi wao. (Imeandaliwa na K-VIS Blogs)
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Vincent Mashinji
Mbunge wa Goba John Mnyika
COMMENTS