MWILI WA MAREHEMU JOSEPH SENGA WAANGWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM LEO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO                                                   ...





JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO

                                                 



                      

   
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA FAMILIA YA JOSEPH EMILIO SENGA.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb) ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Joseph Emilio Senga na wanahabari wote nchini kufuatia kifo cha aliyekuwa mpiga picha mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima na mwanahabari mkongwe Joseph Emilio Senga kilichotokea tarehe 27 Julai, 2016 nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa moyo.
Katika salamu zake Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb) amesema tasnia ya habari imempoteza mtu aliyetoa mchango mkubwa katika kuleta maendeleo ya tasnia ya habari nchini.
“Joseph Senga alikuwa mwanahabari shupavu na hodari, ambaye siku zote alisimama kidete kupigania maendeleo ya tasnia ya habari na kutenda haki katika tasnia hiyo.
“Napenda kutoa  salamu zangu za pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wote wa marehemu”
Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb)  pia amewaombea wote walioguswa na kifo cha Joseph Emilio Senga kuwa na moyo wa subira na uvumilivu katika kipindi hiki cha kuondokewa na mpendwa wao.
RAHA YA MILELE UMPE EHE BWANA, NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE
APUMZIKE KWA AMANI
AMINA.

 Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Joseph Senga liwa katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri jijini Dar es salaam wakati wakiamuaga kwenda Kwimba, Mwanza kwa Maziko. Mwili wa Marehemu Joseph Senga unatarajiwa kuzikwa mara baada ya kufika. 
 Jeneza la Mwili wa Joseph Senga likipewa heshima ya mwisho.
 Wanahabari waliofika kumuaga mwenzao.
 Mpiga Picha Mkuu wa Kampuni ya The Guardiun, Suleiman Mpochi akitoa salamu za rambirambi.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akiteta jambo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye wakati wakiwa kwenye shughuli ya kuaga Mwili wa Aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, Marehemu Joseph Senga, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam leo.
 Mhariri Mtendaji wa Gazeti ya Tanzania Daima, Neville Meena akizungumza.
 Familia ya Marehemu Joseph Senga ikiwa ni yenye huzuni kubwa kuondokewa na Mpendwa wao.
 Mbunge wa Jimbo la Kibamba, John Mnyika akitoa salamu za Rambirambi.
 Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Said Kubenea akizungumza.
 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akizungumza.
  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akitoa salamu.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Baadhi ya Wapiga Picha wa Vyombo mbalimbali vya Habari nchini, wakibeba Jeneza la Marehemu Joseph Senga wakati wakilipeleka kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda Kwimba, Jijini Mwanza kwa Mazishi.














COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MWILI WA MAREHEMU JOSEPH SENGA WAANGWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM LEO
MWILI WA MAREHEMU JOSEPH SENGA WAANGWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM LEO
https://docs.google.com/drawings/u/0/d/sPWCPUxUD3uvN_93UctTQhg/image?w=244&h=141&rev=1&ac=1
https://lh5.googleusercontent.com/qcvjFuVRwAY-OusE8_cROuaWM2dFPCJ0QRTbs4C53H7LsYNz7pJFDoxlOGUu-WjD5AuH_H2SEJidy5hF_kntaxUC3KUfuIxhSpILOjrZOmZGpeqsJRXa5F-W_IIhcT-6pDuk8k5paMT57O9kXg=s72-c
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2016/07/mwili-wa-marehemu-joseph-senga-waangwa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/07/mwili-wa-marehemu-joseph-senga-waangwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy