Promota wa mchezo w masumbwi nchini Haruna Mussa 'Dippo' katikati akizungumza na mashabiki wa mchezo wa ngumi...
Mabondia Halima Bandola (kushoto) na
Joyce Awino wakitunisha misuli mbele ya mashabiki wa mchezo wa masumbwi wakati wa tambulisho wa mpambano wao utakaofanyika Agost 7 katika uwanja wa ndani wa taifa
Joyce Awino wakitunisha misuli mbele ya mashabiki wa mchezo wa masumbwi wakati wa tambulisho wa mpambano wao utakaofanyika Agost 7 katika uwanja wa ndani wa taifa
Promota wa mchezo w masumbwi nchini Haruna
Mussa 'Dippo' akizungumza na mashabiki wa mchezo wa ngumi za kulipwa
wakati alipowatambulisha kupigana kwa mabondia wa kike Halima Bandola (kushoto) na
Joyce Awino watakao oneshana umwamwamba Agost 7 katika uwanja wa ndani
wa Taifa
Promota wa mchezo w masumbwi nchini Haruna
Mussa katikati akiwainua juu mabondia mbele ya mashabiki wa mchezo wa ngumi za kulipwa
wakati alipowatambulisha kupigana kwa mabondia wa kike Halima Bandola na
Joyce Awino watakao oneshana umwamwamba Agost 7 katika uwanja wa ndani
wa Taifa. (Picha SUPER D BOXING NEWS)
Na Mwandishi Wetu
MABONDIA wa kike katika mchezo wa ngumi za kulipwa nchini Halima Bandola na Joyce Awino watapanda ulingoni Agost 7 katika ukumbi wa uwanja wa ndani wa taifa Dar es Salaam kuzichapa.
Akizungumza na mashabiki wa mchezo wa masumbwi wishoni mwa wiki iliyopita promota wa mpambano huo Haruna Mussa 'Dippo' amesema ameamua kuwa promoto wa mabondia wa kike kwa ajili ya kuhamasisa wasichana kuupenda na kuucheza mchezo wa masumbwi kwani kwa sasa michezo ni ajira kwa vijana
Aliongeza kwa kusema katika mpambano huo kutakuwa na mpambano wa kukata na shoka ambapo mabondia Kalama Nyilawila atavaana na Selemani Galile mpambano wa raundi kumi katika uzito wa Kg 72
Mchezo mwingine utakuwa ni kati ya Meshack Mwankemwa kutoka Mbeya atakumbana na Selemani Zugo mpambano wa ubingwa wa Kg 66 raundi kumi
Katika
Mchezo huo kutakua na Uuzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi
pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na
kocha 'Super D'
kwa ajili ya kuwapa mabondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki
kujua sheria za masumbwi.
COMMENTS