WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameondoka jana kwenda Gaborone, Botswana kuhudhuria Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali ...
Mhe. Waziri Mkuu anamuwakilisha Mhe.
Rais Dk. John Pombe Magufuli kwenye mkutano huo utakaofanyika katika Kituo cha
Mikutano cha Kimataifa cha Gaborone (GICC).
Mkutano huo utafunguliwa na Rais wa
Jamuhuri ya Botswana Mhe. Lt. Jen. Seretse Khama Ian Khama ambaye ni SADC,
utajadili hali ya siasa, ulinzi na usalama nchini Lesotho. Mkutano huu
utatanguliwa na Mkutano wa Makatibu Wakuu ambao utafanyika leo
(Jumatatu, 27 Juni, 2016).
Pia mkutano huo utahudhuriwa na Marais
wa Afrika Kusini, Mwenyekiti aliyetoka (outgoing chair) wa Asasi ya Siasa
Ulinzi na Usalama Mhe. Jacob Zuma , Mhe. Jacinto Filipe Nyusi, Rais wa Jamuhuri
ya Msumbiji na Mwenyekiti wa Asasi ya SADC ya Siasa, Ulinzi na Usalama.
Wengine ni Mfalme Mswati III, Mfalme wa
Swaziland ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa SADC, Mhe. Robert Mugabe, Rais wa
Jamhuri ya Zimbabwe na Mwenyekiti anayeondoka wa SADC.
Waziri Mkuu amefuatana na Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dk. Augustine Mahiga,
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi
Dk. Aziz Mlima
na Maofisa wengine waandamizi.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM.
JUMATATU, JUNI 27, 2016.
COMMENTS