Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Juni, 2016 amewaapisha wakuu wa Mikoa watatu aliowa...
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe
29 Juni, 2016 amewaapisha wakuu wa Mikoa watatu aliowateua Jumapili
iliyopita tarehe 26 Juni, 2016.
Wakuu wa Mikoa walioapishwa leo
Ikulu Jijini Dar es salaam ni Dkt. Binilith Satano Mahenge ambaye ni
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dkt. Charles Ogesa Mlingwa ambaye ni Mkuu wa
Mkoa wa Mara na Bi. Zainab Rajab Telack ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga.
Hafla ya kuapishwa kwa wakuu hao wa Mikoa
imehudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu
Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na
wakuu wa wilaya wateule ambao waliteuliwa na Rais Magufuli Jumapili
iliyopita tarehe 26 Juni, 2016.
Aidha, miongoni mwa wakuu wa
wilaya 139 walioteuliwa, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya
mabadiliko madogo katika wilaya tatu ambapo ametengua uteuzi wa Mkuu wa
Wilaya ya Rombo Mteule Mhe. Fatma Hassan Toufiq na badala yake amemteua
Bi. Agness Elias Hokororo kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo, ametengua uteuzi wa
Mkuu wa wilaya ya Serengeti Mteule Bw. Emile Yotham Ntakamulenga na
badala yake amemteua Bw. Nurdin Hassan Babu kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo na
ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mteule Bw. Fikiri Avias
Said na badala yake amemteua Bw. Miraji Mtaturu kuwa Mkuu wa wilaya
hiyo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewataka wakuu wa wilaya wateule
kwenda kuchapa kazi na kutatua kero za wananchi katika wilaya zao huku
wakizingatia kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu.
Rais
Magufuli pia amewataka kusimamia ukusanyaji mapato ya serikali na
matumizi ya fedha na rasilimali nyingine za umma, kuhakikisha wananchi
wapo salama na pia kuhakikisha wananchi wanafanya kazi za uzalishaji
mali.
"Katika kazi hizi wapo watakaowakejeli, katika kazi hizi
wapo watakaowadhihaki, nyinyi kavumilieni na mmuweke Mungu mbele na
mkawaweke watanzania mbele, mkafanye kazi kadiri Mungu atakavyokuwa
amewaongoza.
"Nataka kuwahakikishia tunawaunga mkono kwa nguvu
zote, mkafanye kazi bila uwoga wowote, katembeeni kifua mbele, kwa
sababu tumewaamini wala msiwe na wasiwasi, ukifanya kitu kizuri kwa
dhamira yako iliyo njema kitazaa matunda mazuri, ukifanya kitu kwa
unafiki hakitafanikiwa" Amesema Rais Magufuli
Katika hafla hiyo,
wakuu wa mikoa walioapishwa na wakuu wa wilaya wateule wamekula kiapo
cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma, zoezi ambalo limeongozwa na
Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Salome Kaganda.
Katika hatua
nyingine, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli amekutana na kufanya Mazungumzo na mwenyekiti mwenza wa taasisi
ya Bill and Melinda Gates ya Marekani Bi. Melinda Gates ambapo Rais
Magufuli amemuhakikishia mwenyekiti mwenza huyo kuwa serikali ya awamu
ya tano itaendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano wake na taasisi hiyo
ambayo imekuwa ikishirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi
mbalimbali ya Afya, Uongozi na Kilimo.
Kwa upande wake Bi.
Melinda Gate amempongeza Rais Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya katika
kukabiliana na rushwa na kuongeza ukusanyaji wa mapato ya serikali, na
pia kwa nia yake thabiti ya kuinua sekta ya kilimo inayotegemewa na
idadi kubwa ya watanzania na ameahidi kuwa taasisi ya Bill and Melinda
Gates itaendelea kushirikiana na Serikali ya awamu ya tano katika
kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao ya kilimo.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
29 Juni, 2016 .
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha
Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa mkuu wa mkoa wa Ruvuma Ikulu jijini
Dar es Salaam. |
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi
vitendea kazi Dkt. Binilith Mahenge baada ya kumwapisha kuwa mkuu wa
mkoa wa Ruvuma Ikulu jijini
Dar es Salaam. |
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akimuapisha
Dkt. Charles Mlingwa kuwa mkuu wa mkoa wa Mara Ikulu jijini Dar es
Salawanaoshuhudia ni Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi na Naibu Katibu wa Baraza la Mawaziri, Hassan Shebuge. (Picha zote na Robert Okanda)
|
Rais
Dkt. John Magufuli akitia sahihi kiapo cha
Zainab Telack Mkuu mpya wa mkoa wa Shinyanga baada ya kumwapisha Ikulu jijini Dar es
Salaam leo. |
|
|
Dkt. Charles Mlingwa mkuu mpya wa mkoa wa Mara. |
|
Zainab Telack mkuu wa mkoa wa Shinyanga akiwa katika hafla ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es
Salaam leo. |
|
Zainab Telack mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dkt. Charles Mlingwa (katikati) na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Dkt. Binilith Magenge wakiwa katika hafla ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es
Salaam leo. |
|
Dkt. Binilith Satano Mahenge mkuu wa mkoa wa Ruvuma akiwa katika hafla ya kuapishwa Ikulu
Dar es Salaam leo. |
|
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiongea na Wakuu wa Mikoa pia Wakuu wa Wilaya wakati wa hafla hiyo. |
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
na Wakuu wa mikoa pamoja na Wakuu wa Wilaya wateule mara baada ya
kumaliza kuwaapisha wakuu wa mikoa ya Shinyanga, Mara na Ruvuma Ikulu
jijini Dar es Salaam. |
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
na Wakuu wa mikoa pamoja na Wakuu wa Wilaya wateule mara baada ya
kumaliza kuwaapisha wakuu wa mikoa ya Shinyanga, Mara na Ruvuma Ikulu
jijini Dar es Salaam. |
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dkt. John Pombe Joseph Magufuli,
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa
Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI, Mhe George Simbachawene, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhandisi Mussa Iyombe wakiwa
na sehemu ya Wakuu wapya wa Wilaya waliofika Ikulu jijini Dar es salaam
leo Juni 29, 2016 kula kiapo cha maadili ya viongozi kabla ya kwenda
kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao vya kazi |
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dkt. John Pombe Joseph Magufuli,
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa
Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI, Mhe George Simbachawene, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhandisi Mussa Iyombe wakiwa
na sehemu ya Wakuu wapya wa Wilaya waliofika Ikulu jijini Dar es salaam
leo Juni 29, 2016 kula kiapo cha maadili ya viongozi kabla ya kwenda
kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao vya kazi |
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dkt. John Pombe Joseph Magufuli,
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa
Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI, Mhe George Simbachawene, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhandisi Mussa Iyombe wakiwa
na sehemu ya Wakuu wapya wa Wilaya waliofika Ikulu jijini Dar es salaam
leo Juni 29, 2016 kula kiapo cha maadili ya viongozi kabla ya kwenda
kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao vya kazi |
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakiwa tayari kwa kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi.
|
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakiwa tayari kwa kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi. |
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakiwa tayari kwa kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi. |
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi. |
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi. |
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi.
|
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi.
|
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi.
|
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi.
|
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi.
|
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi.
|
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi mbele ya Kamishna wa maadili ya
Utumishi wa Umma nchini Tanzania Jaji Mstaafu Salome Kaganda (kushoto) waliofika
Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni 29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu
wa Mikoa katika vituo vyao vya kazi.
|
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela baada kuwaapisha Wakuu wa mikoa mara baada ya
kumaliza kuwaapisha wakuu wa mikoa ya Shinyanga, Mara na Ruvuma Ikulu
jijini Dar es Salaam. |
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakiwa tayari kwa kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi. |
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro baada kuwaapisha Wakuu wa mikoa mara baada ya
kumaliza kuwaapisha wakuu wa mikoa ya Shinyanga, Mara na Ruvuma Ikulu
jijini Dar es Salaam. |
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi.
|
|
Wakuu wa wilaya
wapya wakila kiapo cha maadili ya viongozi Ikulu jijini Dar es Salaam leo Juni
29, 2016 kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa Mikoa katika vituo vyao
vya kazi.
|
COMMENTS