Na Greyson Mwase, Dar es Salaam Bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi katika bandari ya Tanga nchini Tanzania linataraj...
Na Greyson Mwase, Dar es
Salaam
Bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda
hadi katika bandari ya Tanga nchini
Tanzania linatarajiwa kukamilika mwezi
Juni mwaka 2020.
Hayo yalielezwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanyika kwa mkutano kati yake
na Waziri wa Nishati na Maendeleo ya
Madini Nchini Uganda, Mhandisi Irene
Muloni aliyeambatana na ujumbe
wake katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam
Lengo la mkutano huo lilikuwa ni kujadili
mpango wa mradi wa ujenzi wa bomba
la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi katika bandari ya
Tanga nchini Tanzania ambapo
ulikutanisha wataalam kutoka nchi zote mbili, ambao ni wa
ardhi, miundombinu, maji, ujenzi, uchumi,, maji barabara pamoja na
makampuni ya mafuta.
Profesa Muhongo alisema kuwa mara baada ya marais wa Tanzania na Uganda kukubaliana kuanza kwa ujenzi wa bomba
la mafuta, kinachofuatia ni utekelezaji
wa kasi ya ajabu ambapo tayari wameanza kukutana na kuunda
kamati ndogo ndogo zitakazokuwa na wataalam mbalimbali kwa ajili
ya kuanza mara moja kwa utekelezaji wa
mradi huo.
Profesa Muhongo alisema kuwa serikali
za nchi zote mbili zimejipanga katika kuhakikisha kuwa ujenzi huo unakwenda kwa kasi kubwa, ikiwezekana ujenzi ukamilike mwishoni
mwa mwaka 2019.
Aliongeza kuwa serikali ya Uganda inatarajia kujenga kiwanda kwa
ajili ya kusafisha mafuta ghafi Hoima
ambapo wametoa hisa 40 zenye
thamani ya Dola za Marekani bilioni 4.7 kwa nchi zilizomo ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo kila nchi itaweza
kununua asilimia nane ya hisa hizo na kusisitiza kuwa Tanzania ipo
tayari kununua hisa nane kwa
thamani ya Dola za Marekani milioni 150.4
Aliendelea kusema kuwa hisa zitanunuliwa na
serikali pamoja na wawekezaji binafsi watakaoonesha nia ya kununua hisa ili
waweze kunufaika na mradi huo.
Hata hivyo aliongeza kuwa nchi ya Uganda pamoja na nchi nyingine zilizomo ndani
ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wameomba kununua
gesi kutoka nchini Tanzania na kusema kuwa kwa kuanzia serikali inatarajia kujenga bomba la gesi hadi nchini Uganda ili waweze kunufaika na gesi hiyo.
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akielezea
uzoefu wa Tanzania kwenye ujenzi wa miradi ya mabomba ya gesi na mafuta
katika mkutano huo. Kushoto ni Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini
Nchini Uganda, Mhandisi Irene Muloni na kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara
ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa.
Alisema kuwa bomba la gesi litasambazwa
katika mikoa ya kaskazini na mingineyo ili
uchumi wa nchi uweze kukua kwa kasi na
Tanzania kuwa nchi yenye kipato cha kati ifikapo mwaka
2025 kama Dira ya Maendeleo
ya Taifa inavyofafanua.
“ Kila sehemu
yenye gesi ya kutosha,
lazima tuhakikishe tunaweka bomba la gesi ambalo
ni mkombozi wa uchumi wa nchi,”
alisisitiza Profesa Muhongo.
Wakati huo huo Waziri wa Nishati na
Maendeleo ya Madini Nchini Uganda, Mhandisi Irene
Muloni, aliishukuru serikali ya
Tanzania kwa kuwa tayari
kushirikiana na Uganda kwa ajili ya mradi mkubwa wa ujenzi wa bomba la
mafuta.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia madini
Profesa James Mdoe ( wa kwanza kushoto, waliokaa mbele); Naibu Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia nishati Dk.
Mhandisi Juliana Pallangyo ( wa pili kushoto waliokaa mbele) pamoja na
wataalam wengine wa Wizara ya Nishati na Madini wakifuatilia kwa makini
hotuba iliyokuwa inatolewa na Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini
Nchini Uganda, Mhandisi Irene Muloni (hayupo pichani) katika mkutano
kati ya nchi ya Tanzania na Uganda lengo likiwa ni kujadili mpango wa
ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda hadi katika bandari ya
Tanga nchini Tanzania.
Alisema kupitia uzoefu
wa Tanzania katika ujenzi wa
mabomba ya gesi na mafuta pamoja na
wataalam waliobobea anaamini kuwa mradi
huu utakwenda kwa kasi kubwa na kukamilika kwa wakati.
Aliiomba
nchi ya Tanzania pamoja na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na makampuni ya mafuta, jamii itakayopitiwa na
miundombinu ya bomba la mafuta kutoa ushirikiano ili mradi
uweze kukamilika kwa wakati kama ilivyopangwa.
Alisema kuwa
mkutano wa pili unatarajiwa
kufanyika Hoima nchini Uganda tarehe
27 Mei, mwaka huu na kuendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali yatakayopitiwa na bomba la mafuta.
Wataalam
kutoka Wizara, taasisi na makampuni ya mafuta kutoka Tanzania na Uganda
wakifuatilia kwa makini mada iliyokuwa inawasilishwa na mwakilishi
kutoka kampuni ya Total katika mkutano huo.
Aidha
ameipongeza Tanzania katika kuwa sehemu ya watekelezaji wa mradi huo na
kuahidi kuendelea na ushirikiano katika miradi mingine.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Maendeleo ya Madini Nchini Uganda, Dk.
Fred Kaliisa (kushoto) akifafanua jambo katika kikao hicho. Kulia ni
Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Nchini Uganda, Mhandisi Irene
Muloni.
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza na
waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta
kutoka Hoima nchini Uganda hadi katika bandari ya Tanga nchini Tanzania.
Kulia ni Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Nchini Uganda,
Mhandisi Irene Muloni.
Waziri
wa Nishati na Maendeleo ya Madini Nchini Uganda, Mhandisi Irene Muloni
(kulia) akifafanua jambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari
mara baada ya kukamilika kwa mkutano huo. Kushoto ni Waziri wa Nishati
na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Balozi wa Uganda Nchini Tanzania, Dorothy Hyuha akifafanua jambo katika mkutano huo.
COMMENTS