PROF. MBARAWA AWATAKA POSTA NA TTCL KUFANYA BIASHARA

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa tatu kulia) akipata maelezo ya namna mitambo ya Kampuni ya Sim...









Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa tatu kulia) akipata maelezo ya namna mitambo ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) inavyofanya kazi kutoka kwa Mtaalamu wa Mitambo (Technician) Edward Lukungu (wa pili kushoto) wakati wa ziara ya kutembelea Shirika hilo jijini Mwanza.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (kushoto) akipata taarifa ya utendaji wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) kutoka kwa Meneja Mkoa wa Mwanza, Julius Chifungo wakati alipotembelea ofisi za Shirika hilo jijini Mwanza. Kulia ni Meneja wa TTCL Mkoa wa Mwanza, Johnbosco Kalista.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akiangalia moja ya mitambo ya mkongo wa taifa iliyopo Mkoani Mwanza.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa menejimenti ya TTCL na Posta alipowatembelea jijini Mwanza.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akiongea na wafanyakazi (hawapo pichani) kuhusu kufanya kazi kwa uadiliafu na uwazi ili kusaidia mashirika hayo kusonga mbele.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akifafanua jambo kwa wafanyakazi wa TTCL na POSTA mara baada ya kutembelea na kuona utendaji kazi wao, jijini Mwanza.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akisalimiana na watumishi wa TTCL na Posta mkoani Mwanza.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano).
************************

Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame  Mbarawa amewataka watendaji wa Shirika la Posta Tanzania na   Kampuni ya simu ya (TTCL) kufanya kazi kwa weledi na mtazamo  wa kibiashara  ili kuyaongezea mapato mashirika hayo na hivyo  kuendana na  mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanaoyotokea nchini.
Akizungumza na wafanyakazi wa TTCL na POSTA mkoani Mwanza Prof. Mbarawa amesema kutokana na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano duniani biashara simu na posta hivi sasa ina ushindani mkubwa unaohitaji mtazamo mpana wa kibiashara ili kukidhi mahitaji ya soko.
“Serikali inajitahidi kuisaidia TTCL na POSTA hivyo wekezeni vizuri kwenye data na uharaka wa utoaji huduma ili muweze kushindana kwenye soko na kukuza uchumi wa taasisi hizi muhimu kwa usitawi wa nchi”, amesema Prof Mbarawa.
Prof. Mbarawa amezitaka menejimenti za POSTA na TTCL kufanya kazi kwa uwazi na uadilifu ili malengo na mikakati ya taasisi hizo yafahamike kwa wafanyakazi wote na kuwezesha kujipima kama wanafikia malengo yaliyokusudiwa.
“Hakikisheni wafanyakazi wote wanaelewa malengo na mikakati ya tasisi zenu ili kazi ya kuyatekeleza ifanywe kwa umoja na ushirikiano”, amesisitiza Waziri Prof. Mbarawa.
Aidha, Waziri Prof. Mbarawa amesisitiza umuhimu wa wafanyakazi kuwa wadilifu na kuepuka kuwa mawakala wa mashirika mengine na hivyo kuihujumu Serikali.
“kuna watu ndani ya TTCL na POSTA ambao ni wazembe, wavivu na wanao hujumu Serikali tutawaondoa mara moja, Ni vema kubaki na wafanyakazi wachache waadilifu kuliko wengi wasiotimiza maelngo yaliyokusudiwa”, amefafanua Waziri Prof. Mbarawa
Naye Meneja wa TTCL mkoa wa Mwanza Bw. Johnbosco Kalista amemweleza Waziri Mbarawa kuwa wigo wa mtandao kutofikia walaji wengi, wateja kutolipa madeni kwa wakati na ulinzi na usalama wa miundombinu ya mawasiliano ni miongoni mwa changamoto zinazoikabili shirika hilo mkoani Mwanza.
 Kwa upande wake Meneja wa POSTA mkoa wa Mwanza, Julius Chifungo amebainisha kuwa uchakavu wa barabara, maslahi yasiyokidhi ya wafanyakazi na uchakavu wa majengo ni miongoni mwa vikwazo vinavyoathiri utendaji kazi wa shirika hilo mkoani Mwanza.
Takribani masanduku elfu tisa yanasimamiwa na Shirika la Posta mkoani Mwanza katika ofisi zake kumi na moja na asilimia 96.8 hukodishwa na kuingizia shirika hilo faida, Wakati takriban wateja 45,041 wanahudumiwa na TTCL katika Mkoa wa Mwanza.

(Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano).

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: PROF. MBARAWA AWATAKA POSTA NA TTCL KUFANYA BIASHARA
PROF. MBARAWA AWATAKA POSTA NA TTCL KUFANYA BIASHARA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgNf3v7PAMJziib5Vyaqj2Ws4OfEJxv8TNwFrY_dSXykDwFvrjtGsvRK1J5gsICfJg1YjpEqS-25VUngASNLg7ZQIQrweU8DTtv3tzEfxmVAQZjqT-LIkhjZJWwUVpY7VzyWLyEgXuHl5gm/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgNf3v7PAMJziib5Vyaqj2Ws4OfEJxv8TNwFrY_dSXykDwFvrjtGsvRK1J5gsICfJg1YjpEqS-25VUngASNLg7ZQIQrweU8DTtv3tzEfxmVAQZjqT-LIkhjZJWwUVpY7VzyWLyEgXuHl5gm/s72-c/1.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2016/02/prof-mbarawa-awataka-posta-na-ttcl.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2016/02/prof-mbarawa-awataka-posta-na-ttcl.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy