WAZIRI MKUU AALIKA WAWEKEZAJI KUTOKA VIETNAM

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Mizengo Pinda akizungumza katika hafla ya maadhimisho ya Miaka 50 ya Mahusi...








Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Mizengo Pinda akizungumza katika hafla ya maadhimisho ya Miaka 50 ya Mahusiano ya Kidiplomasia kati ya Tanzania na Vietnam. Katika hotuba yake Mhe. Pinda alilishukuru Taifa la Vietnam kupitia Ubalozi wake nchini kwa kuendelea kuimarisha ushirikiano  na Tanzania katika nyanja mbalimbali zikiwemo za kiuchumi, biashara na kidiplomasia. Hafla hiyo ilifanyika katika Hotel ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 02 Septemba 2015.
Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Vothanh Nam naye akizungumza katika hafla hiyo.
Afisa Mambo ya Nje Bw. Emmanuel Luangisa (katikati) akifuatilia hotuba kwenye kitabu iliyokuwa ikisomwa na Mhe. Waziri Mkuu (hayupo pichani) 
Waziri Mkuu, Mhe. Pinda (kulia) na Balozi wa Vietnam nchini Mhe. Vothanh Nam (kushoto) wakitakiana afya njema  kwenye hafla hiyo. 
Waziri Mkuu akitakiana afya njema na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Yahya Simba (wa pili kutoka kulia). Mwenye nguo nyekundu  ni Mke wa Balozi wa Vietnam nchini  na kulia ni Afisa kutoka  Ubalozi wa Vietnam nchini. 
Mhe. Pinda akikata Keki pamoja na Balozi Nam ikiwa ni ishara ya kuadhimisha miaka 50 ya ushirikiano wa Kidiplomasia kati ya Tanzania na Vietnam. 
Balozi wa Vietnam, Mhe. Nam (kulia) akimpokea Waziri Mkuu, Mhe. Pinda (kushoto) alipowasili kwenye maadhimisho hayo anayeshuhudia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Balozi Yahya Simba
Mhe. Pinda (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mindi Kasiga.
Waziri Mkuu, Mhe. Pinda akisalimiana na raia wa Vietnam waishio nchini waliojitokeza kumpokea alipowasili kwenye maadhimisho hayo.
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda (kulia) na Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Vothanh Nam (kushoto) wakiwa wamesimama kwa pamoja tayari kwa nyimbo za mataifa yao.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Yahya Simba (wa pili kutoka kulia) kwa pamoja na Mke wa Balozi wa Vietnam nchini na Kiongozi wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini ambaye pia ni Balozi wa Demokrasia ya Kongo nchini Balozi Juma Mpango (kushoto) wakiwa wamesimama wakati nyimbo za taifa la Tanzania na Vietnam zikiimbwa. 
Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini nao wakiwa wamesimama tayari kwa kuimba  nyimbo za Taifa
Kikundi cha Polisi cha Brass Band kikipiga nyimbo za Mataifa hayo mawili wakati wa Maadhimisho hayo
Sehemu ya wageni waalikwa kwenye maadhimisho hayo.
Maafisa kutoka Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nao wakiwa na nyuso za furaha wakati wa maadhimisho hayo. 
(Picha na Reginald Philip)








WAZIRI MKUU AALIKA WAWEKEZAJI KUTOKA VIETNAM



WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema wakati Tanzania inajiandaa kutekeleza awamu ya pili ya mpango wa maendeleo wa miaka mitano (2016 -2020) ambao unalenga kukuza viwanda nchini, haina budi kuangalia ni aina gani ya uwekezaji unafaa kuchukuliwa kwa manufaa ya nchi.



Ametoa kauli hiyo jana usiku (Jumatano, Septemba 2, 2015), wakati akizungumza na mabalozi na wageni mbalimbali waliohudhuria maadhimisho ya miaka 70 ya Uhuru wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam na miaka 50 ya kuanzishwa kwa mahusiano ya kidiplomasia baina ya Tanzania na Vietnam, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.



“Huu ni wakati muafaka kwa nchi zetu kuangalia ni aina zipi za uwekezaji zinafaa kuchukuliwa kwa manufaa ya nchi zetu na wananchi wake. Nitumie fursa hii kuwakaribisha wawekezaji kutoka makampuni ya Ki-Vietnam waje kuwekeza kwenye usindikaji wa korosho, utengenezaji wa saruji na viwanda vya nguo,” alisema.



Aliyataja maeneo mengine ambayo wenye makampuni wanaweza kuwekeza kuwa ni nyanja ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) pamoja na ujenzi wa nyumba za kuishi (real estate development).



Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuipongeza kampuni ya mawasiliano ya simu ya Vietnam (VIETTEL) kwa uamuzi wake wa kutenga dola za Marekani bilioni moja ambazo zitatumika kuendesha shughuli zake hapa nchini.



“Huu ni mtaji mkubwa sana, siyo tu hapa Afrika Mashariki na Kati bali hata barani Asia. Uwekezaji huu utazalisha ajira za moja kwa moja 1,700 na ajira nyingine 20,000 ambazo si za moja kwa moja,” aliongeza.



Kwa upande wake, Balozi wa Vietnam nchini Tanzania, Bw. Vo Thanh Nam alisema tangu ipate uhuru wake hadi, nchi hiyo imekwishaanzisha mahusiano ya kidiplomasia na nchi 185 na wakati huo huo imekwishaweka mahusiano ya kibiashara na uwekezaji na nchi 220. “Vietnam ni mwanachama hai katika mashirika ya kimataifa na kikanda zaidi ya 70 yakiwemo UN, WTO, ASEAN NA APEC,” alisema.



Akizungumzia kuhusu miaka 50 ya mahusiano ya kidiplomasia baina ya Vietnam na Tanzania, Balozi Thanh Nam alisema mbali ya kujenga mahusiano ya kijamii, kisiasa na kiuchumi, nchi hizo mbili zimeunganishwa na uwekezaji uliofanywa na kampuni ya VIETTEL GROUP kwenye sekta ya mawasiliano.



Hafla hiyo ilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Yahaya Simba na mabalozi wa nchi mbalimbali wakiongozwa na Balozi Juma Alfani Mpango, ambaye ni Mkuu wa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MKUU AALIKA WAWEKEZAJI KUTOKA VIETNAM
WAZIRI MKUU AALIKA WAWEKEZAJI KUTOKA VIETNAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghjcoFiJGX0GwP39GczIFWvpocMOhvHCEw-7tG0d9YX2Q7n6pkXLbIsnv4ONgD6QOsTe6fvJTINlopeuEKCM9BfUSAwwGhy8vnX0-vmJZhXZbun7qI-f_pCaS1_veZnvLKJugEHl_oprs/s640/SAM_0445.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghjcoFiJGX0GwP39GczIFWvpocMOhvHCEw-7tG0d9YX2Q7n6pkXLbIsnv4ONgD6QOsTe6fvJTINlopeuEKCM9BfUSAwwGhy8vnX0-vmJZhXZbun7qI-f_pCaS1_veZnvLKJugEHl_oprs/s72-c/SAM_0445.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2015/09/waziri-mkuu-aalika-wawekezaji-kutoka.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2015/09/waziri-mkuu-aalika-wawekezaji-kutoka.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy