Skauti wa shule ya Kimataifa ya Joyland, wakiruka sarakasi wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigambo...
|
Skauti wa shule ya Kimataifa ya Joyland,
wakiruka sarakasi wakati wa mahafali ya
pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam |
|
Wahitimu wa masomo ya awali shule ya
Kimataifa ya Joyland, wakiimba wimbo wa Shule wakati wa mahafali ya pili ya
shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam |
|
Wanafunzi
shule darasa la nne shule ya Kimataifa ya Joyland, wakiimba wimbo wa shule wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni
jijini Dar es Salaam. |
|
Wahitimu wa masomo ya awali shule ya
Kimataifa ya Joyland, wakiimba wimbo wa shule wakati wa mahafali ya pili ya
shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam. |
|
Wanafunzi
wa darasa la awali shule ya
Kimataifa ya Joyland, wakiimba wimbo
wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni
jijini Dar es Salaam. |
|
Wanafunzi
wa darasa la awali shule ya
Kimataifa ya Joyland, wakiimba wimbo
wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni
jijini Dar es Salaam. |
|
Mkurugenzi wa shule ya Kimataifa ya Joyland, Fedrick
Otieno akiwasaidia watoto wa darasa la awali kupanda juu ya jukwaa kuimba wimbo
maalum wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni
jijini Dar es Salaam |
|
Mhitimu wa masomo ya awali shule ya Kimataifa
ya Joyland, Colin Christopher akisoma hotuba wakati wa mahafali ya pili ya
shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam |
|
Mkaguzi Mkuu wa Elimu Kanda, Shani Kanungira akitoa
hotupa ya awali kabla ya mgeni rasmi wakati wa mahafali ya pili ya shule hiyo
iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam |
|
Mwakilishi wa Afisa Elimu ya Msingi Manispaa
ya Temeke, Frank Makingi akizungumza Tuangoma Kigamboni Dar es Salaam wakati wa
mahafali ya pili ya shule hiyo |
|
Wanafunzi wa darasa pili shule ya Kimataifa ya
Joyland, wakicheza ngoma ya utamaduni (Ndolela) wakati wa mahafali ya pili ya
shule hiyo iliyopo Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam |
|
Mkurugenzi wa shule ya Kimataifa ya Joyland, Fedrick
Otieno akitoa neno la shukrani. |
|
********************** |
WAZAZI wamehimizwa kujenga utamaduni wa kupitia kazi na watoto wao
wanaporudi shuleni kwa lengo la kusaidia ufahamu wao na kuwarahisishia
kazi walimu katika suala la taaluma.
Pia wamekumbushwa kufuatilia
nyendo za watoto wao kujua wanacheza wapi, na akina nani na rafiki gani
wanaokuwa nao kwa muda mrefu sambamba na kutowaachia kutumia muda mrefu
kwenye runinga kwani ni moja ya sababu ya kuharibika kwao na kuporomoka
kimasomo wawapo likizoni.
Wito huo ulitolewa na Mkurugenzi wa Shule
ya Kimataifa ya Joyland, Fredrick Otieno wakati wa mahafali ya wanafunzi
wa masomo ya awali wa shule hiyo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki
shuleni hapo, Tua Ngoma, Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Otieno
alisema ushirikiano wa wazazi na walimu katika malezi ya watoto ni
msaada mkubwa wa wanafunzi, lakini kama wazazi na walezi wataliacha
jukumu hilo kwa walimu tu ni mtihani mkubwa na kuchangia kuporomoka kwa
kiwango cha elimu nchini. Alisema ni lazima wazazi na walezi wakague
madaftari na kazi za watoto wao wawapo majumbani na pia kuwazuia kuingia
katika makundi au kuumia muda mrefu kucheza wakati wa likizo ili
viwango vyao kitaaluma visiporomoke.
Pia aliwakumbusha wazazi na
walezi kujenga tabia ya kuwalipa ada watoto wao ili kurahisisha kazi kwa
shule wanazosoma kuwa kile kinachostahiki, alisema kucheleweshwa kwa
ada ni tatizo ambalo linapunguza morali wa kazi kwa walimu, ingawa
alisema Joyland imekuwa ikijitahidi kuhakikisha wanafunzi wanakipata
kile kilichowapeleka wakati wazazi na walezi wakikumbushwa wajibu wao wa
kuwalipia ada.
Mkurugenzi huyo alisisitiza kuwa hakuna hazina bora
kama mtoto kupewa elimu ambayo huja kumsaidia ukubwani kwa kuzingatia
kuwa dunia ya sasa inaendeshwa kisasa na bila elimu bora na ya kutosha
ni vigumu kijana kusimama na kukabiliana na changamoto hizo.
Naye
Mkaguzi Mkuu wa Elimu Kanda, Shani Kanungira aliwasisitiza wazazi
kutumia kujitolea na kutimiza wajibu wao kuwasomesha watoto badala ya
kutumia fedha nyingi kwa mambo yasiyo na tija kwa watoto na familia zao
kwa ujumla.
Shani alitoa nasaha yake kabla ya kumpisha Mwakilishi wa
Afisa Elimu ya Msingi Manispaa ya Temeke, Frank Makingi aliyesisitiza
umuhimu wa wazazi na walezi kujenga utamaduni wa ushirikiano dhidi ya
walimu wa shule wanazosoma watoto wao.
Makingi alisema siyo kila
jambo la wanafunzi kuachwa mikononi mwa walimu tu, kadhalika alikumbusha
kuwasaidia watoto katika kuwalea katika maadili mema ili kulifanya
taifa kuwa na raia wema na viongozi wazuri na waadilifu wa baadaye
COMMENTS