Sehemu ya WanaCCM na wakazi wa Mji wa Morogoro, wakiwa wamekusanyika nje ya Ofisi za CCM Mkoa huo, kumlaki Waziri Mkuu Mstaa...
Sehemu ya WanaCCM na wakazi wa Mji wa Morogoro, wakiwa wamekusanyika nje ya Ofisi za CCM Mkoa huo, kumlaki Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa, pindi alipowasili kwenye ofisi hizo kukabidhiwa
orodha ya majina ya WanaCCM waliomdhani ili apate ridhaa ya chama chake
kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika
Oktoba 25, 2015. Mh. Lowassa amehitimisha zoezi hilo la kutafura
Wadhamini, Juni 29, 2015 katika Mkoa wa Morogoro na amedhaminiwa na
WanaCCM 104,038.
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini,
Fikiri Juma, pindi alipowasili kwenye Ofisi za CCM Mkoa wa Morogoro, leo
Juni 29, 2015 kwa ajili ya kukabidhiwa
orodha ya majina ya WanaCCM waliomdhani ili apate ridhaa ya chama chake
kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika
Oktoba 25, 2015. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Innocent
Kalageris. Mh. Lowassa amehitimisha zoezi hilo la kutafura Wadhamini, Juni 29, 2015 katika Mkoa wa Morogoro na amedhaminiwa na WanaCCM 104,038. PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
Mapokezi ya Mh. Lowassa Mkoani Morogoro.
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akisaini kitabu cha wageni kwenye Ofisi za CCM Mkoa wa Morogoro,
leo Juni 29, 2015. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Innocent Kalageris na kushoto ni Mke wa Mh. Lowassa, Mama Regina Lowassa. Mh. Lowassa amehitimisha zoezi hilo la kutafura Wadhamini, Juni 29, 2015 katika Mkoa wa Morogoro na amedhaminiwa na WanaCCM 104,038.Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiwapungia WanaCCM wa Mkoa wa Morogoro wakati alipowasili tayari kwa kukabidhiwa orodha ya majina ya WanaCCM waliomdhani ili apate ridhaa ya chama chake kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Mh. Lowassa amehitimisha zoezi hilo la kutafura Wadhamini, Juni 29, 2015 katika Mkoa wa Morogoro na amedhaminiwa na WanaCCM 104,038.
Umati wa WanaCCM wa Mkoa wa Morogoro ukiwa umefurika kwa wingi wake kwenye viwanja vya CCM Mkoa wa Morogoro, kumsikiliza Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa.
WanaCCM wa Mkoa wa Morogoro wakifatilia kwa makini.
Mzee
Steven Mashishanga akiyarudi magoma kabla ya kupanda jukwaani kuzungumza
machache na kuwasalimia WanaCCM wa Mkoa wa Morogoro.
Mzee Steven Mashishanga akizungumza machache na kuwasalimia WanaCCM wa Mkoa wa Morogoro.
Dkt. Juma Ngasongwa akitoa neno.
Mh. Lowassa akipena mkono na Dkt. Juma Ngasongwa.
Askofu Mamio akisalimia.
Wadau Mkutanoni.
Mwenyekiti
wa Wenyeviti wa CCM kutoka Zanzibar, Mzee BoraAfya akitoa salamu zake
kwa WanaCCM wa Mkoa wa Morogoro waliokuwa wamekusanyika kwenye Uwanja wa
CCM Mkoa huo, Juni 29, 2015.
Mzee Msindai katika ubora wake.
Mke
wa Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania,
Mh. Edward Lowassa, Mama Regina Lowassa akiwasalimia WanaCCM wa Mkoa wa
Morogoro, Juni 29, 2015.Taswira mbalimbali za WanaCCM wa Mji wa Morogoro Mjini na maeneo ya jirani katika zoezi la kupokea orodha ya majini ya WanaCCM waliomdamini Mh. Edward Lowassa.
Wapiga picha wakitafuta taswira zilizo bora kabisa.
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa akifatilia kwa makini taarifa ya Katibu wa CCM Wilaya ya
Morogoro Mjini, Kulwa Mironge wakati akitaja idadi ya WanaCCM
waliomdhamini. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Innocent Kalageris.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam, Salum Madenge akisalimia wanaCCM wa Mkoa wa Morogoro.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akifurahia jambo.
Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa, Mama Regina Lowassa akifurahia jambo.
Mwenyekiti
Mstaafu wa CCM Mkoa wa Morogoro, Kanali Mstaafu Isack Mwisongo
akizungumza jambo na kutoa historia kidgo ya Chama cha Mapinduzi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Innocent Kalageris akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward
Lowassa, kutoa shukrani zake kwa wanaCCM waliomdhamini.Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akipokea orodha ya majina ya WanaCCM waliomdhani ili apate ridhaa ya chama chake kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015, kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Kulwa Mironge. Mh. Lowassa amehitimisha zoezi hilo la kutafura Wadhamini, leo Juni 29, 2015 katika Mkoa wa Morogoro na amedhaminiwa na WanaCCM 104,038.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akionyesha fomu yenye orodha ya majina ya wanaCCM waliomdhamini, kwa kadamnasi iliyokuwepo kwenye Uwanja wa CCM Mkoa wa Morogoro, Juni 29, 2015, baada ya kukabidhiwa na Katibu wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Kulwa Mironge.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza machache na kutoa shukrani kwa WanaCCM waliomdhanini ili apate ridhaa ya chama chake kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.
(Imeandaliwa na Michuzi blogs) |
COMMENTS