WATU wanne wanaosadikiwa kuwa majambazi, wamekamatwa na polisi jijini Dar es Salaam, mapema leo Jumanne Aprili 21, 2015, baada ...
|
WATU
wanne wanaosadikiwa kuwa majambazi, wamekamatwa na polisi jijini Dar es Salaam,
mapema leo Jumanne Aprili 21, 2015, baada ya kutuhumiwa kumpora Mzungu mmoja kwenye barabara ya Kinondoni jirani na benki
ya Stanbic.
Vyanzo
vya uhakika kutoka polisi vimeiambia K-VIS BLOG kuwa, watu hao waliokuwa na
silaha, walifanya uporaji huo, na kuondoka wakiwa kwenye gari dogo Toyota SIENTA
yenya namba za usajili T787 DBU, na kuondoka wakielekea barabara ya Ali Hassan
Mwinyi uelekeo wa Posta
Hata
hivyo
mtu mmoja ambaye aliona uhalifu huo aliwafuata bila ya majambazi hayo
kujua huku akiwa
ametoa ripoti polisi na walipofika jirani na makutano ya barabara za
bibititi Mohammed na Ali Hassan Mwinyi raia huyo mwema aliwakinga kwa
mbele na hapo ikawa kama sinema, kwani majambazi hayo haraka haraka
yalishuka na bunduki na k kwa nia ya kumtisha ili awapishe, hata hivyo
jaribio lao hakufua dafu, kwani askari wa pikipiki walivamia eneo hilo
kama nyuki na kuwaweka chini ya ulinzi. Haraka haraka, polisi waliwatia
pingu na kuwaamuru kulala chini huku wakilipekua gari hilo na kukuta
silaha ndani yake. Kwa
sasa tayari wako mikononi mwa polisi.
|
|
Polisi wakikagua gari la watuhumiwa hao. (Source; K-VIS Blogs) |
COMMENTS