Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma na kikundi cha ngoma cha Msanja group kabla ya kuhutubia mamia ya wakazi wa...
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma na kikundi cha ngoma cha Msanja group kabla ya kuhutubia mamia ya wakazi wa Usangi kuhusu ujenzi wa barabara ya Kikweni-Usangi-Lomwe ambayo itaanza kujengwa hivi karibuni. |
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli
(katikati) akiweka jiwe na msingi kuashiria kuanza kwa ujenzi wa barabara ya
Mwanga-Kikweni-Vuchama-Usangi-Lomwe yenye urefu wa Kilomita 40. Kushoto (kwake) ni
Waziri wa Maji ambaye pia ni Mbunge wa Mwanga, Profesa Jumanne Maghembe, Mkuu wa
Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama (wa pili kulia) pamoja na viongozi wengine wa Wilaya ya
Mwanga.
Waziri wa Ujenzi Dkt.
John Pombe Magufuli (kushoto) akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya
Ujenzi Eng. Musa Iyombe kabla ya kuweka jiwe la msingi katika barabara ya
Mwanga-Kikweni-Vuchama-Usangi-Lomwe yenye urefu wa Kilomita 40.6. Katikati ni Waziri
wa Maji ambaye pia ni Mbunge wa Mwanga Profesa Jumanne Maghembe.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama wakicheza ngoma na kikundi
cha ngoma za asili Kikweni kabla ya uzinduzi wa barabara ya Mwanga-Kikweni-Vuchama-Usangi-Lomwe
yenye urefu wa Kilomita 40.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli
(katikati) akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mhe.
Ana Kilango Malecela katika sehemu ya Kihurio. Dkt Magufuli ametangaza kujengwa Kilometa tatu za lami katika eneo hilo pamoja na kuifanyia maandalizi ya
kujengwa kwa kiwango cha lami barabara ya Mkomazi-Same yenye urefu wa Km 96.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwahutubia
mamia ya wakazi wa Kihurio Same Mkoani Kilimanjaro.
Wakazi wa Usangi waliojitokeza kumsikiliza
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli
Waziri wa Ujenzi, Dkt John Magufuli akiwahutubia wakazi wa Gonja
wakati akipita kukagua barabara ya Kihurio hadi Gonja maore Wilayani Same
Mkoani Kilimanjaro.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na
wananchi wa Usangi mara baada ya kuwahutubia.
Picha ya Pamoja Waziri
wa Ujenzi Dkt. John Magufuli (katikati) akiwa pamoja na Waziri wa Maji, Profesa
Jumanne Maghembe (wa pili kulia), Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama (kulia), pamoja na Viongozi
wengine wa Wilaya na Chama cha Mapinduzi mara baada ya kuhitimisha ziara yake
katika Wilaya za Same na Mwanga mkoani Kilimanjaro. (Picha zote kwa Hisani ya
Kitengo cha Mawasiliano-Wizara ya Ujenzi)
COMMENTS