GLOBAL HEALTH CATALYST CANCER SUMMIT 2015 AT HAVARD MEDICAL SCHOOL

Mhe. Liberatus Mulamula Balozi wa Muungano ya Jamhuri ya Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberatus Mulamula, alipozung...








Mhe. Liberatus Mulamula

Balozi wa Muungano ya Jamhuri ya Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberatus Mulamula, alipozungumza  katika kongamano  la mapambano dhidi ya gojwa la saratani duniani, aliwataka wanaDiaspora wa nchi za kiAfrika kuwa mstari wa mbele kwa kushirikiana na watalaamu wa vitengo vya afya duniani ili kuboresha upatikana wa huduma za afya barani Afrika. 
Mhe. Balozi Mulamula, ambaye pia ndie aliyekuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo alizungumzia faida za kutumia Teknolojia  ili kuboresha mawasiliano kati ya wataalam, utafiti na  elimu . 
Nia mojawapo ya  kongamano la Global Health Catalyst Cancer Summit 2015 ni kuboresha huduma mahiri za saratani barani Afrika kwa  kutumia ( Information and Communication Technologies (ICTs);Teknolojia ya mawasiliano kati ya wataalam wa gojwa la saratani wa nchi za nchi za ng'ambo  na wataalam waliopo barani Afrika.Mhe. Balozi L. Mulamula, alikabidhi Tunzo Maalum kwa Bigwa wa Tiba ya Saraatani Dr. Twalibu Ngoma. Dr.Ngoma ni miongoni mwa wataalam wa kuigwa ambaye amepata elimu ya juu nje ya nchi na kureja nyumbani ili kuboresha upatikanaji wa huduma na elimu ya saratani nchini Tanzania
 Dkt. Twalibu Ngoma
Profesa na Mkuu wa Kituo cha Kliniki ya Mafunzo ya Sarataani kilichopo University ya Muhimbili Dar es Salaam nchini Tanzania
       Mhe. Balozi Mulamula na Watanzania wanaDiaspora wakimpongeza Dkt. Ngoma kwa furaha

Uniting Africans in Diaspora (AID)  Against Cancer;
Sehemu ya pili  ya kongamano la Global Health Catalyst cancer  Summit ilijumuisha wanaDiaspora waafrika  ambao ni nguvu kubwa na rasilimali endelevu kwa katika nchi zao za kuzaliwa. Ripoti ya utafiti uliofanywa kwa baadhi ya viongozi wa  USA Afrikan Diaspora imedhihirisha kuwa karibu asilimia 90 % ya wanadiaspora wana nia na malengo ya kuleta mabadiliko katika nyanja mbali mbali nchini mwao ukiwemo uwanja wa afya  barani afrika.
Dr. Doyin Oluwole
      Mkurugenzi wa Taasisi ya Pink Ribbon Red Ribbon, jitihada zilizoanzishwa na   Rais  Mstaafu 
                                                              Mhe. George W. Bush 
Mashirika mbalimbali yalionyesha  mipango ya ujenzi wa vituo vya kutoa tiba ya saratani nchin Tanzania

Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV, Mhe. Iddi Sandaly alieleza nia ya wanaDaspora kuwa mstari wa mbele katika kuboresha upatikanaji wa huduma za afya  nchini Tanzania na malengo ya kupeleka huduma ya afya kwa jamii zenye uhitaji  hivi karibuni.

Mabigwa wa Saaratani mbalimbali duniani wakijadili njia bora  za kuborehsa huduma za saratani.

Ukosefu wa Elimu Afya kwa jamii ni kati ya changamoto zinazopelekea ongezeko la vifo vya gojwa la saratani barani Afrika. Saratani nyingi huweza kutibika endapo zimegundulika mapema na kupata utafiti na huduma sahihi.


Mwanzilishi wa http://www.nesiwangu.com/ ; mtandao unahusika na utoaji wa Elimu Afya kwa lugha ya kiswahili  Bi. harriet Shangarai, alizungumzia faida za kutoa Elimu Afya kwa kutumia lugha ya asilia na  kusema kuwa baadhi ya wasomaji wake walitafuta huduma ya haraka baada kujisomea na  kuelewa dalili  zenye kuashiria hitilafu katika mifumo mbali mbali mwilini. Bi. Harriet alizungumzia faida zitokanazo na Teknolojia ya mawasiliano ambayo ni fursa kubwa kwa Wanadiaspora kutoa mchango wao wa kielimu kwa jamii na kujenga mawasilino ya karibu na wataalam wa afya nchini mwao ili kwa pamoja waweze kushirikiana katika  kuziba  mapengo yaliyomo kwenye uwanja wa huduma na elimu ya afya.

Wataalam wa afya katika diaspora walipata fursa ya kujadili njia mbali mbali zitakazowawezesha kushirikiana  na kupata  fafanuzi za huduma za afya nchini mwao.


        Taasisi binafsi na vyombo mbali mbali vinavyotumika kuboresha huduma za saratani barani Afrika
                                Afrikan Women cancer Awareness association (AWCAA)


Mkurugenzi na Mwanzilishi wa African Women Cancer Awearness association NGO ( AWCAA)
Mrs.Ify Nwobuke (kushoto) na Mwakilishi wa AWCAA (kulia),  walizungumzi huduma za saratini ya matiti  mbazo wamekuwa wakizitoa barani Afrika. Mrs Ify alisema saratani ya matiti yaweza kutibika iwapo imegunduika mapema hivyo elimu kwa jamii ni muhimu katika mapambano ya saratani.

Shukrani;
Waandalizi wa Global Health Catalyst Cancer Summit @ Harvard Medical School, 2015
Kwa maelezo zaidi pitia

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: GLOBAL HEALTH CATALYST CANCER SUMMIT 2015 AT HAVARD MEDICAL SCHOOL
GLOBAL HEALTH CATALYST CANCER SUMMIT 2015 AT HAVARD MEDICAL SCHOOL
https://lh6.googleusercontent.com/-2ghF101_95g/VRcIpuQABKI/AAAAAAAAC7w/A2JDJhxJydc/s640/DSCN4339.JPG
https://lh6.googleusercontent.com/-2ghF101_95g/VRcIpuQABKI/AAAAAAAAC7w/A2JDJhxJydc/s72-c/DSCN4339.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2015/03/global-health-catalyst-cancer-summit.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2015/03/global-health-catalyst-cancer-summit.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy